BEKI Branislav Ivanovic anatakiwa na Monaco baada ya kumkosa Vincent Kompany kutoka Manchester City.
Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 29 wa 
Chelsea amependekezwa na kocha Claudio Ranieri kwa mmiliki bilionea wa 
Kirusi, Dmitry Rybolovlev katika mpango wa kuijenga timu hiyo iliyopanda
 Ligi Kuu Ufaransa iwe tishio.
Walitoa oda ya Pauni Milioni 51.3 
iliyokubaliwa na Atletico Madrid kwa mshambuliaji Radamel Falcao, ambaye
 anatarajiwa kufanyiwa vipimo leo, baada ya Ijumaa kukamilisha mpango wa
 kuwasajili kwa Pauni Milioni 60 wachezaji wawili wa Porto, Joao 
Moutinho na James Rodriguez.

Katika rangi ya bluu? Branislav Ivanovic anatakiwa kwa udi na uvumba na Monaco

Monaco ipo tayari kutoa kiasi cha Pauni 
Milioni 25 kumnasa Ivanovic, ambaye alifunga bao la ushindi katika 
fainali ya Europa League, lakini pia anatakiwa na kocha mpya wa Chelsea,
 Jose Mourinho. 
'Special One' alijaribu kumsajili 
Ivanovic msimu uliopita akiwa bado Real Madrid lakini akakwama baada ya 
Chelsea kupandisha bei yake, na atataka Mserbia huyo aendelee kuwa 
sehemu ya kikosi cha msimu ujao. 
Pamoja na hayo atapenda kumsajili 
Raphael Varane wa Real Madrid na beki ambaye Mourinho anaweza kumuacha 
ni David Luiz, ambaye anatakiwa na Barcelona.
Monaco pia inamtaka Hatem Ben Arfa wa Newcastle.




0 comments:
Post a Comment