Wednesday, July 3, 2013

Kaseja+na+Kim 
Na Baraka Mpenja 
Wanandinga wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha Mdenish Kim Paulsen wanatarajiwa kuingia kambini leo katika hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam kujiandaa na mechi dhidi ya Uganda, The Cranes kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza mecihi ya kukata na mundu dhidi ya wapinzani wao wa karibu, timu ya Taifa ya Uganda Julai 13 mwaka huu, saa 9:00 Alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye mjini Kampala, nchini Uganda.
Katika kikosi hicho, kocha Kim Paulsen amemteua kipa Juma Kaseja kuwa kipa namba moja na nahodha wa timu hiyo licha ya klabu yake ya Simba “Taifa kubwa” kutangaza kuachana naye.
Kim akiongea na waandishi wa habari siku ya jana alisema Kaseja bado ana kiwango cha juu na anafanya kazi yake vizuri akiwa langoni, hivyo ni lazima awepo katika kikosi chake na kuwa kiongozi.
“Kaseja ni kipa mzuri, anafanya kazi nzuri kwa timu ya taifa, hivyo nimemuita katika kikosi changu. Atakuwa kipa namba moja na nahodha. Mimi sijali kilichotokea klabuni kwake, hayanihusu. Ninachojua bado huduma yake ni nzuri na ndio maana nimemteua na ataendelea kuwa kiongozi kama kawaida”. Alisema Kim.
Siku za karibuni Kim alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa, ameshangazwa na klabu ya Simba kumtema Kaseja kwani bado ni mlinda mlango bora kwa sasa nchini Tanzania na hakuna kipa mzuri kama yeye kwa sasa.
Kim alisema Kaseja ana uwezo mkubwa, pia ni kiongozi mzuri akiwa uwanjani, hivyo ni jambo la ajabu kwa Simba kumuacha kipa huyo.
Wakati Kim akisema hayo, nao viongozi wa Simba walisema kuwa Kaseja alikuwa na nyodo sana, mara kadhaa walimuita aende ofisini kuzungumza na viongozi kuhusu hatima yake ya mkataba ambao ulimazika klabuni hapo, lakini kipa huyo hakuonesha ushirikiano kwa madai kuwa ana majukumu ya timu ya taifa.
Baada ya kumaliza majukumu ya timu ya taifa, bado Kaseja aliweka ngumu kutokea mezani, na ndipo viongozi wa Simba wakaamua kuachana naye kwa madai kuwa labda ana mipango mingine.
Lakini bado Kocha wa Stars ameponda maamuzi ya kuachwa kwa Kaseja, na kama sehemu ya kumuamini sana, Jana ametangza kikosi chake na Kaseja ni kipa namba moja na atakuwa nahodha.
Wachezaji walioteuliwa na Kocha Mdenmark, Kim Poulsen  ni makipa Juma Kaseja (Simba) , Aishi Manula (Azam), Mwadini Ally (Azam) na Ally Mustafa (Yanga). Mabeki ni David Luhende (Yanga SC), Aggrey Morris (Azam), Shomary Kapombe (simba), Erasto Nyoni (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondan (Yanga),  Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haroun Chanongo (Simba), Juma Luizio (Mtibwa Sugar),  Mudathiri Yahya (Azam), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), (Simba),
Washambuliaji ni Simon Msuva (Yanga), Mrisho Ngassa (Simba), John Bocco (Azam).
Kwasasa Stars inatupian jicho la tatu katika fainali za CHAN baada kutupwa nje ya michuano ya kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia nchini Brazil mwakani baada ya kufungwa na Ivory Coast juni 16 uwanja wa taifa mabao 4-2 na kupoteza matumaini.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video