Wednesday, July 3, 2013

bingwa 
Na Baraka Mpenja 
Mabingwa watetezi wa soka Tanzania bara, wanajangwani Dar Young Aficans, “Kwalalumpa Malysia” wanaendelea kujifua katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola, Mabibo jijini Dar es salaam ikiwa ni maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu unaotarajiwa kuanza kushika kasi Agosti 24 mwaka huu pamoja na michauno ya kimataifa mwakani.
Afisa habari wa klabu ya Yanga, Baraka Kizuguto amezungumza na mtandao wa MATUKIO DUNIANI na kusema kuwa kwa sasa ndio wameanza mazoezi chini ya kocha Mholanzi Ernie Brandts, hivyo kikubwa mashabiki na wanachama wa klabu hiyo waungane pamoja wakati huu wa maandalizi kwani ndio msingi wa kufanya vizuri.
“Tumeanza mazoezi vizuri, tunamshukuru sana mungu mazoezi yanakwenda barabara, lakini kuna watu wanaandika mambo yao kuwa kuna wachezaji hawapo, kikubwa watu wawe wanauliza kwanini wachezaji hawapo, sio kuzungumza tu. Wachezaji wana bosi wao ambaye ni kocha, wajenge utamaduni wa kuuliza ili wapewe sababu”. Alisema Kizuguto.
Kizuguto alisema malengo yao ni kujiweka sawa kutetea ubingwa wao pamoja na kufanya vizuri katika mitanange ya ligi ya mabingwa barani Afirika tofauti na miaka ya nyuma, na ndio maana wameamua kukazia zaidi mazoezi ya mapema.
Pia afisa habari huyo alisema ratiba yao ya kwenda mikoani iko palepale, na Ijumaa ya kesho kutwa wataanza safari ya kuelekea kanda ya ziwa jijini Mwnaza ambapo wataonana na mashabiki wao ili kuwaonesha kombe lao walilotwaa msimu ujao.
“Kikubwa kwa sasa tunafanya mazoezi, lakini keshokutwa tunaelekea Mwanza kama tulivyoeleza awali, hakuna kilichoharibika kwa sasa”. Alisema Kizuguto.
Kuhusu Yanga kususia hafla ya ugawaji wa zawadi inayoendeshwa na wadhamini wa ligi kuu Tanzania bara, kampuni ya simu ya Vodacom inayotarajiwa kufanyika leo, Kizuguto alisema maelekezo yao yako palepale na msimamo ni ule ule.
“Tunahitaji watufanyie huduma ile ya kutuhamisha pea kabisa, leo hii wanaonesha mfano wa hundi, tunataka kuona hela yetu imeingia katika akaunti yetu na baada ya hapo tutashiriki pamoja nao. Lakini kinyume na hivyo sisi hatutashiriki kwani mfano wa hundi haina maana yoyote kwetu”. Alisema Kizuguto.
Yanga walitangaza kususia hafla ya kugawa zawadi za washindi wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita kwa madai kuwa wadhamini hao wamechelewa sana ukizingatia ligi ilimalizika tangu mei 18 mwaka huu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video