![]()  | 
| Kijikio | 
Maafande
 wa Ruvu Shooting chini ya kocha Charles Boniface Mkwasa “Masta” 
wamendelea kutangaza vita kwa klabu za ligi kuu Tanzania bara msimu 
ujao, hususani Simba, Yanga na Azam fc.
Afisa
 habari wa klabu hiyo Masau Bwire ameuambia mtandao wa MATUKIO DUNIANI kuwa 
msimu ujao wa ligi kuu hakuna kulala, watapambana kufa na kupona 
kuhakikisha wanapata nafasi tatu za juu.
Masau
 alisema katika kuhakikisha wanafanikisha doto yao wameendelea kufanya 
vizuri katika usajili na mpaka sasa wamepata nyota watano.
Mchezaji
  Juma Seif Dion ‘Kijiko’, aliyekuwa akiichezea Africon Lyon msimu 
uliyopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara naye amejiunga na Ruvu Shooting ya 
Pwani kwa mkataba wa miaka miwili.
Kijiko
 aliyewahi pia kukipiga Yanga, alisaini mkataba huo  hivi karibuni 
katika ofisi za timu hiyo Mlandizi, Kibaha tayari kuitumikia kwa msimu 
ujao.
Kijiko
 ni mchezaji wa tano kusaini mkataba na timu hiyo kwa ajili ya msimu 
mpya wa ligi, wengine waliosaini ni Ciosmas Ader (Azam), Elias Maguli 
(Prison), Juma Nade (Kagera Sugar) na Lambale Jerome (Ashanti).
Wakati
 huo huo, uongozi wa timu hiyo ya Ruvu Shooting umetangaza kuwaacha 
wachezaji watano kutokana na kiwango chao cha kucheza mpira kushuka.
Ofisa
 Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, aliwataja wachezaji hao kua ni 
Pail Ndauka, Charles Nobart, Gido Chawala, Frank Mabande na Liberatus 
Manyasi.
Kwa 
mujibu wa Bwire, timu hiyo tayari iko kambini kikosi cha Jeshi 832 Ruvu 
JKT, itaanza mazoezi rasmi siku ya Jumatatu, Juni 24 chini ya Kocha 
Mkuu, Charles Mkwasa.
Bwire
 amewataka wachezaji wote ambao kawajaripoti kambini wafike haraka kabla
 ya Jumatatu ikiwa ni pamoja na wachezaji wapya waliosajiliwa msimu huu.


0 comments:
Post a Comment