Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
KOCHA Andre Villas-Boas ameripotiwa kupiga chini ofa ya kuifundisha Paris Saint-Germain ili abaki Tottenham.
 Mabingwa
 hao wa Ufaransa walitaka Mreno huyo arithi mikoba ya Carlo Ancelotti, 
anayeelekea Real Madrid, lakini sasa wamehamishia mawindo yao kwa Fabio 
Capello.
 Inafahamika
 Villas-Boas alipewa ofa ya Mkataba wa miaka mitatu na mabilionea wa 
Qatari wanaoimiliki PSG baada ya majadiliano na wakala wake, Carlos 
Goncalves, lakini mwalimu huyo kijana wa miaka 35 anataka kufanya mambo 
adimu Spurs waliomchukua msimu uliopita baada ya kutupiwa virago 
Chelsea.
 Tottenham
 wanatarajiwa kubomoa benki kumpa fedha za kutosha Villas-Boas, 
aliyebakiza miaka miwili katika Mkataba wake White Hart Lane, ili 
kujenga kikosi cha nguvu cha kukata tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa.
 Miongoni
 mwa wachezaji anaowataka ni kiungo wa Corinthians, Paulinho, wakati 
Spurs pia ni klabu pekee iliyoomba kumsajili kiungo wa Atletico Mineiro,
 Bernard. Wakala wake amesema: “Dortmund hawajawasilisha mapendekezo na 
Tottenham ni washindani pekee,”.
 Villas-Boas
 pia inaelezwa anavutiwa na ushindani wa kupambana na bosi wake wa 
zamani, Mreno mwenzake Jose Mourinho katika Ligi Kuu England msimu ujao 
 Anabaki: Villas-Boas ameripotiwa kubaki White Hart Lane
 
 Kazi ya kufanya: Villas-Boas anataka kuipaisha matawi ya juu zaidi Spurs kutoka nafasi ya tano aliyowapa msimu uliopita
 
 Mpango B: Kocha wa Urusi, Capello anaweza kuwa kazini msimu ujao
Taarifa
 za jana usiku nchini Ufaransa zinasema kocha wa zamani wa England, 
Capello atakuwa mwalimu mpya wa PSG kwa Mkataba wa mwaka mmoja
 Kocha wa zamani wa England, Capello anatazamiwa kuwa mpango B wa PSG, licha ya kwamba bado ana Mkataba wa mwaka mmoja Urusi.
 Urusi
 ipo kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Dunia 
mwakani nchini Brazil,na kuna uwezekano Capello akarejea katika timu 
hiyo ya taifa baada ya msimu mmoja na PSG kukamilisha majukumu yake 
katika Kombe la Dunia.

 Carlo Ancelotti anatarajia kuhamia Real Madrid

 Msimu mzuri: PSG walikuwa mabingwa Ufaransa na wanataka kujiimarisha zaidi




0 comments:
Post a Comment