Tuesday, April 9, 2013



Na Baraka Mpenja
Kufuatia mchezo wa riadha kushuka nchini, Chama cha riadha mkoani Pwani kwa kushirikiana na chama cha riadha Tanzania (RT) kinaendesha mafunzo  maalumu ya kufundisha kozi za ukocha wa mchezo huo zinazoendelea mjini Kibaha mkoani Pwani.
Akizungumza na mtandao huu kutoka Kibaha, mmoja wa wakufunzi  wa mafunzo hayo , katibu mkuu wa RT Suleiman Nyambui amesema mafunzo hayo yana lengo la kupata wataalamu mbalimbali nchini Tanzania.
“Riadha ni miongoni mwa michezo mashuhuri duniani, ukirudi miaka ya sabini, Tanzania ilikuwa inaogopeka kimataifa katika mchezo huu, nadhani unawakumbuka akina Bayi na Nyambui, sasa tunataka kurudisha hadhi ya mchezo huu unaozidi kushuka”. Alisema Nyambui.
Katibu huyo wa RT alisema kuwa mafunzo hayo yanayoendelea kibaha yamejumuisha waalimu kutoka mikoa ya Songea, Geita, Mara, Morogoro, Rukwa huku waalimu wengi wawakitokea mkoa wa Pwani.
Nyambua aliongeza kuwa leo walikuwepo  madaktari wa viungo  kutoka wizara ya Vijana, utamaduni na michezo ambao wamefundisha namna ya kugundua na kuwatibu wanariadha wapatapo majeruhi.
Mafunzo hayo yatamalizika jumamosi ya wiki hii kwa wahitimu hao kutunukiwa vyeti katika hafla maalumu itakayoandaliwa mjini Kibaha.
Akizungumzia mkakati wa RT, Nyambui alisema kuwa ifikapo mwaka 2020 watahakikisha kila shule Tanzania ina mwalimu mtaalamu wa kufundisha riadha kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Nyambui alisisitiza kuwa suala hilo litafanikiwa kwa kushirikiana na viongozi wa serikali, wadau wa michezo na watanzania wote kwa ujumla.
“Tukikubali umuhimu wa mchezo huu kwa taifa,tutaweza kufika mbali na kuwafikia wenzetu wa Ethiopia, Kenya na wengine ambao wanafanya vizuri zaidi katika mchezo huo”. Alisema Nyambui.
Katibu huyo alisema wakati huu si mwafaka kuandaa timu kwa ajili ya Olmpiki wala michuano yoyote ya kimataifa, bali ni wakati wa kufumbia macho michuano hiyo ili nafasi ya kujenga misingi ya mchezo huo ipatikane.
Nyambui aliongeza kuwa kwa sasa wanajipanga kuzunguka mikoa yote ili waongea na maafisa michezo, pamoja na maafisa elimu ili kila shule iwe inafundisha riadha.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video