Tuesday, April 9, 2013


MAN_UNITED_WAKISHANGILIA_ETIHAD>>MKAZO MECHI ZIJAZO: STOKE, WEST HAM & VILLA!!
Sir Alex Ferguson amedai Manchester United walikosa ‘bahati’ kwa kufungwa 2-1 na Manchester City hapo jana na pia alikiri kuwa, Siku zote, Timu yake ‘hujibebesha zigo’ badala ya kurahisisha kazi.
Ingawa jana walifungwa, Man United bado wapo kileleni wakiwa Pointi 12 mbele ya Man City na Mechi zikiwa zimebaki 7.
Kwa hali ilivyo sasa, Man United wanahitaji kushinda Mechi 3 na Sare 1 kati ya hizo Mechi zao 7 ili watwae Ubingwa ikiwa Man City watashinda Mechi za mbele yao.
+++++++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Man Utd
31
38
77
2
Man City
31
30
65
3
Chelsea
31
28
58
4
Tottenham
32
15
58
5
Arsenal
31
27
56
6
Everton
31
12
52
7
Liverpool
32
19
49
+++++++++++++++++++++++++++++++
Akiongelea Mechi hiyo ya jana, Ferguson alidokeza Bao la kwanza la Man City lililofungwa na James Milner lilikuwa na ukiukwaji kwani kulikuwa na Ofsaidi.
Ferguson alieleza: “Tevez alikuwa akiingilia mchezo na alikuwa Ofsaidi. Alikuwa akimziba Kipa na kama hiyo si kuingilia mchezo, sasa sijui ni nini!”
Ferguson pia alipuuzia pale alipoambiwa kuwa kuongoza kwa Pointi 15 kuliwafanya Man United wabweteke na kucheza kichovu katika Mechi ya jana hasa Mkongwe Ryan Giggs ambae ndie alipoteza Mpira uliozaa Bao la kwanza.
Akipuuza dhana hiyo, Sir Alex Ferguson amesema mkazo wao sasa ni kushinda Mechi ijayo watakayocheza ugenini Jumapili na Stoke City na Siku 3 baadae wapo tena ugenini huko Upton Park kucheza na West Ham na kufuatia Mechi ya Nyumbani Old Trafford dhidi ya Aston Villa.
Alisema: “Hatutabweteka. Ukiangalia Historia ya Klabu hii, kwa Miaka mingi tumekuwa tukijipa ugumu wenyewe na kuwaacha Mashabiki wetu roho mkononi! Lakini tunaongoza kwa Pointi 12 na bado zipo Mechi 7 tu. Kila gemu tunayocheza, unapunguza Mechi. Mkazo wetu sasa ni Stoke hapo Jumapili.”
MANU UNITED-MECHI ZILIZOBAKI:
Jumapili Aprili 14
[Saa 10 Dak 5 Jioni]
Stoke V Man Utd
Jumatano Aprili 17
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
West Ham V Man Utd
Jumatatu Aprili 22
[Saa 4 Usiku]
Man Utd V Aston Villa
Jumapili Aprili 28
[Saa 12 Jioni]
Arsenal V Man Utd
Jumamosi Mei 4
[Saa 11 Jioni]
Man Utd V Chelsea
Jumapili Mei 12
[Saa 11 Jioni]
Man Utd V Swansea
Jumamosi Mei 19
[Saa 12 Jioni]
West Brom V Man Utd

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video