
Na Baraka Mpenja
Mabingwa
mara mbili wa kombe la mapinduzi na wawakililishi pekee wa Tanzania
katika michuano ya kimataifa wana lambalamba Azam fc kesho wanashuka
dimbani kuwakabili waarabu kutoka nchini Morroco timu ya jeshi ya AS FAR
Rabat katika mchezo wa kombe la shirikisho raundi ya tatu.
Mchezo huu wa kukata na shoka utapigwa uwanja wa taifa majira tya saa kumi kamili kwa saa za Afrika mashariki.
Leo
hii Makocha wa timu za Azam, Sterwat John Hall na wa FAR Rabat,
Abderazzak Khairi watakutana na waandishi wa habari kuzungumzia mechi
hiyo.
Mkutano
huo ambao pia utawahusisha manahodha wa timu hizo mbili na utafanyika
saa 5 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
zilizoko Uwanja wa Karume, Barabara ya Uhuru na Shaurimoyo.
Afisa
habari wa klabu ya Azam fc Jafar Idd Maganga aliwata watanzania kuondoa
shaka kwani kikosi chao kipo kamili kado kuwavaa maafande hao kutoka
milima ya Atlas.
Idd aliwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi hapo kesho ili kuwashangilia wawakilishi hao wa taifa katika michuano ya kimataifa.
“Tuondoe
itikadi za klabu, tujumuike kwa pamoja kupata matokeo ya ushindi,
tunawashukuru watanzania watakaojitokeza hapo kesho”. Alisema Idd.
AS FAR Rabat waliwasili jana Dar es Salaam na kufanya vya hapa na pale.
Kwanza walikuwa ni watu wenye wasiwasi tangu wanatua Uwanja wa Ndege na wasiowaamini wenyeji wao, wakitaka zaidi kujiongoza wenyewe na baadaye sasa wakakataa hoteli waliyokodiwa na wenyeji wao, Sapphire Court.
Pamoja na kuambiwa hoteli hiyo imepitishwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na timu zote zilizocheza na Azam katika mashindano hayo, zilifikia hapo, Al Nasir ya Sudan Kusini na Barack Young Controllers II ya Liberia, lakini wakagoma.
Kwanza walikuwa ni watu wenye wasiwasi tangu wanatua Uwanja wa Ndege na wasiowaamini wenyeji wao, wakitaka zaidi kujiongoza wenyewe na baadaye sasa wakakataa hoteli waliyokodiwa na wenyeji wao, Sapphire Court.
Pamoja na kuambiwa hoteli hiyo imepitishwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na timu zote zilizocheza na Azam katika mashindano hayo, zilifikia hapo, Al Nasir ya Sudan Kusini na Barack Young Controllers II ya Liberia, lakini wakagoma.
Wenyeji
wakawaambia kama hawataki hoteli hiyo watajilipia popote watakapokwenda
na Waarabu hao nao wakaonyesha jeuri ya fedha kwa kujipangia New Africa
Hotel. Kaazi kweli kweli.
0 comments:
Post a Comment