Na Baraka Mpenja 
Homa 
ya pambano kali la masumbwi ama ndonga la kuwania ubingwa wa IBF Africa 
baina ya bondia bingwa mtetezi Francis Cheka dhidi ya Thomas Mashali 
“Simba asiyefugika” inazidi kupanda kwa mashabiki wa wanaume hao wenye 
ubora zaidi katika mchezo huo.
Rais wa Kampuni ya ngumi za kulipwa Tanzania Yasin Abdallah “Ustadhi” ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa tayari mabondia wote wapo Dar es salaam na leo hii majira ya saa 
tano asubuhi watapima uzito katika ukumbi wa hoteli ya Nzeka Magomeni 
Kondoa jijini hapa.
“Hakika
 tambo zimetawala kila kona huku mashabiki wa mabondia hao wakitambiana 
kwa hali ya juu, leo hii tunawapima uzito na kesho shughuli yenyewe 
itaanza ukumbi wa PTA kwa wapinzania hao kupanda ulingoni wakitanguliwa 
na mapambano ya utangulizi”. Alisema Yasin.
Akizungumzia
 vipimo vya matumizi ya kuongeza nguvu “Bangi” na mengine mengi, Yasin 
alisema mabondia wote watapimwa na kama kuna bondia atabainika kutumia 
madawa hayo yanayokatazwa michezoni  basi atauza ushindi wake kwa 
mpinzani wake.
Ustadhi
 aliwaomba mabondia wote watakaocheza mapambano ya utangulizi kujitokeza
 mapema ili kukamilisha zoezi la upimaji wa uzito kabla ya kuwapima 
wanaume wawili watakaoshindania gari mpya aina ya Noah.
Kiingilio
 cha chini katika pambano hilo litakalopambwa na mapambano mengi ya 
utangulizi kitakuwa shilingi elfu saba za kitanzania (7000/=).
Yasin
 alisema mashabiki wa mji kasoro bahari Morogoro wamesisitiza kuwa 
hawatakubali kupoteza ubingwa wao na gari mpya, bali watamuunga mkono 
Cheka mwanzo mwisho katika ili achukue tena taji hilo.
Kwa 
upande wa mashabiki wa Mashali wa jijini Dar es salaam wanajigamba kuwa 
 bingwa wa Afrika Mashariki na Kati “Simba asiyefugika” Thomas Mashali 
lazima amtandike Cheka ambaye ni mpinzani wake mkubwa kwa sasa.
Tambo
 zimetawala jijini Dar es salaam huku mashabiki wengi wakimfananisha 
Cheka na timu za Hispania, Barcelona na Real Madrid kuwa ufalme wake 
umefika ukingoni na sasa anavua rasmi taji lake.
Kwa upande wa Cheka ameiambia MICHEZO BOMBA! kuwa amezoea maneno ya wapinzani wake, kwani waliwahi kuongea wengi lakini wakaambualia kipigo cha aibu.
“Niko
 vizuri sana, nimejiandaa kwa umakini mkubwa kutetea ubingwa wangu, 
mashabiki wangu wa Morogoro wananisapoti sana na sitawangusha hata 
kidogo”. Alisema Cheka.


0 comments:
Post a Comment