Wachezaji
 wa klabu ya Yanga ambao ndio mabingwa wa liku kuu soka Tanzania bara 
msimu wa 2012/2013 wakiweka miili sawa, wa kwanza kulia ni kiungo 
tegemeo wa klabu hiyo Mnyarwanda Haruna Hakizima Fadhil Niyonzima 
maarufu kama Fabrigas, naye atakuwepo hapo kesho kupambana na wagosi wa 
kaya 
 
 
Kikosi
 cha Wagosi wa kaya, Wagosi wa Ndima kutoka jiji la Tanga, hawa ndio 
walichangia kuwapa ubingwa Yanga wiki hii baada ya kuwabana Azam, sasa 
wanashuka ugani kesho dhidi ya mabingwa hao
Na Baraka Mpenja 
Wakiwa
 tayari mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2012/2013, 
wanajangwani Dar Young Africans wamesema mchezo wao wa mei mosi dhidi ya
 wagosi wa ndima wagosi wa kaya Caostal Union kutoka jijini Tanga “waja 
leo waondoka leo” ndani ya dimba la kisasa la taifa jijini Dar es salaam
 utakuwa maalumu kwa mashabiki wa klabu huyo kufurahia pamoja ubingwa 
wao huku timu yao ikiwa inaendelea kufanya vizuri.
Afisa habari wa mabingwa hao waliotwa taji mara 24 liku kuu, Baraka Kizuguto ameiambia MICHEZO BOMBA!
 kuwa baada ya kuwapoka ubinwgwa watani zao wa jadi, sasa wanataka 
kuwafurahisha mashabiki wao katika michezo yao miwili iliyosalia.
Yanga
 wamebakiza mechi mbili baina ya Wagosi wa Kaya ambao watakwaruzana nao 
kesho taifa na mchezo wa mwisho utawakutanisha na watani zao wa jadi 
wekundu wa msimbazi Simba wenye kumbukumbu ya kuwachapa kipigo cha mbwa 
mwizi cha mabo 5-0 msimu wa mwaka jana.
“Licha
 ya kuwa mabingwa Yanga hatubweteki hata kidogo, tunaanza kugawa dozi 
kwa wagosi wa kaya na baada ya hapo tunaanza kuwawinda Simba ambao 
kuwafunga itaongeza raha ya ubingwa wetu”. Alisema Kizuguto.
Kuhusu
 hali ya wachezaji, Kizuguto alisema wote wapo salama na wana morali 
kubwa sana kuwavaa wapinzani wao waliochangia kuwapa ubingwa baada ya 
kuwabana waliokuwa wapinzani wao wakubwa Azam fc  “Lambalamba” kwa 
kutoka nao sare ya bao 1-1 dimba la chama cha Mapinduzi (CCM) jijini 
Tanga.
“Tumefanya
 mazoezi vizuri, wachezaji kwanza wana furaha ya kutwaa ubingwa, lakini 
wanaahidi kuwa ili kunogesha utamu wa ubingwa wao lazima washinde kesho 
na mechi ya Simba”. Alisema Kizuguto kwa kujiamini.
Wakati
 Yanga wakitamba kuibuka kidedea hapo kesho, kwa upande wa Coastal union
 wamesema maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Hemed Morroco ameimabia MICHEZO BOMBA!
 kuwa licha ya waamuzi kuvurunda baadhi ya michezo wao wamejipanga kwa 
uzuri sana kukabiliana na Yanga hapo kesho uwanja wa taifa.
“Siku
 tumecheza na Azam nyumbani waamuzi walichemsha sana na kusababisiha 
tushindwe kupata ushindi, hakika tulistahili kuwafunga, sasa tuna kazi 
nyingine na Yanga sijui itakuwaje, lakini tumejipanga kwa lolote lile”. 
Alisema Morroco kwa kujiamini.
Coastal
 union wamejikusanyia pointi 36 katika nafasi ya tano,  juu yao wapo 
Simba wenye pointi  39 katika nafasi ya nne huku Kagera Sugar wakiwa 
nafasi ya tatu na pointi 40  na Azam wapo nafasi ya pili na mzigo wa 
pointi 48.
Kesho
 mashine za Yanga kama Haruna Niyonzima “Fabrigas”, Khamis Kiiza, Saimon
 Msuva, Athman Idd “Chuji”, Frank Domayo, Kelvin Yondan, Canavaro na 
wengine wengi wataongoza kikosi chao kupepetana na Wagosi wa ndima 
kutoka Tanga.


0 comments:
Post a Comment