MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Maalim Seif Sharif Hamad, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi
wa mashindano ya Kombe la Mapinduzi kwenye Uwanja wa Amaan visiwani
Zanzibar, leo.
 |
Maalim Seif Sharif Hamad, |
Kwa mujibu wa Msemaji wa Kamati ya Mashindano, Farouk Karim, ufunguzi
huo unatarajiwa kufanyika usiku na kufuatiwa na mechi kati ya Simba ya
Tanzania bara na Jamhuri ya Pemba.
 |
WEKUNDU WA MSIMBAZI KUTOKA TANZANIA BARA |
|
 |
KIKOSI CHA JAMHURI YA PEMBA KUTOKA VISIWANI ZANZIBAR |
Alisema kuwa, mchezo mwingine hii leo utakuwa kati ya Mtibwa Sugar
dhidi ya Miembeni, ambao utafanyika kwenye uwanja wa Mao Tsetung kuanzia
saa 10 alasiri na kwamba, maandalizi yote yamekamilika, ambapo timu
zote shiriki zimeshaanza kuwasili visiwani humo.
Karim alisema kuwa, Januari 4 kutakuwa na mechi mbili, ambapo Jamhuri
na Bandari zitacheza saa 10 alasiri na saa 2 usiku, Tusker ya Kenya
itakuwa dimbani dhidi ya Simba huku Januari 5, Mtibwa Sugar itapepetana
na Coastal Union saa 10 alasiri, wakati Miembeni na Azam shughuli
itakuwa saa 2 usiku.
Alisema, mechi nyingine zitakuwa kati ya Tusker na Jamhuri saa 10
alasiri na mechi ya mwisho ya kundi hilo itakuwa kati ya Simba na
Bandari wakati kundi B zitakuwa kati ya Miembeni na Coastal Union saa 10
alasiri na mechi ya mwisho katika mzunguko huo wa kwanza ni kati ya
Azam
na Mtibwa Sugar.
Karim aliongeza kuwa, hatua ya nusu fainali itaanza Januari 9 kwa
mchezo mmoja huku wa pili ukiwa ni Januari 10, ambapo mechi zote
zitapigwa saa 2 usiku.
Aliongeza kuwa, fainali za michuano hiyo zitarindima Januari 12 saa 2
usiku, ikiwa ni kilele cha michuano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka.
 |
UWANJA WA AMAN MJINI ZANZIBAR |
0 comments:
Post a Comment