Mabingwa
wa watetezi wa kombe la Kagame,Yanga ya Dar es Salaam leo imeshindwa kuwapa
zawadi ya Krismasi wapenzi na mashabiki wake baada ya kuchapwa bao 1 – 0 dhidi ya Tusker ya Kenya katika mchezo wa
kimataifa wa kirafiki.

Mchezo
huo uliochezwa katika dimba la Taifa ulitumika pia kumtambulisha mchezaji mpya
wa klabu hiyo Kabange Twite ambaye ni pacha wa Mbuyu Twite,pia kuwaaga
mashabiki kabla ya kuelekea Uturuki kwa ajili ya kujifua zaidi kabla ya
michuano ya kombe la Kagame na Mzunguko wa pili wa ligi kuu.
![]() |
WACHEZAJI WA TUSKER |
Tusker
ilifunga goli hilo kwa mkwaju wa penati dakika ya 45 ambapo kipindi cha pili
kocha wa Yanga Ernie Brandts akaamua
kuwaingiza Hamisi Kiiza,Nizar Khalfan,Simon Msuva na Jerryson Tegete lakini
mabadiliko hayo hayakuzaa matunda.
Kwa
mujibu wa Makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga timu ya Yanga inatakiwa
kuelekea Uturuki Desemba 28 mwaka huu tayari kwa maandalizi ya michuano ya
kombe la Kagame na
0 comments:
Post a Comment