Afisa habari wa Azam fc Jafar Idd Maganga, amesema katibu mkuu wa klabu hiyo, Idrisa Nasoro, amemwambia leo kuwa tayari barua ipo na kilichobaki ni kukaa na kujadili ombi hilo.
Idd amesema watakaa muda wowote kuotka sasa na watasema nini maamzi yao juu ya ushiriki wao.
Azam walirejea juzi nchini wakitokea kongo walikoshiriki michuano ya kombe la Hisani la shirikisho la soka nchini Kongo na kutwaa ubingwa wa kombe hilo.
Idd amesema ziara hiyo imewapa maandalizi mazuri ya michuano ya kimataifa na mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara.
0 comments:
Post a Comment