BAADA YA KULOWA DABI YA MBEYA WAKILALA 2-0, MBEYA CITY WAENDELEZA MAWINDO
BAADA ya mapumziko ya saa 24 siku ya jana kupisha dakika 90 za matokeo mabaya dhdi ya Tanzania Prison jumamosi iliyopita, kikosi cha Mbeya City Fc leo kimeanza mazoezi kujindaa na mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara dhidi ya JKT Ruvu uliopangwa kuchezwa jumamaosi ijayo kwenye uwanja wa Sokine jumamosi ijayo.
Akizungumza na mbeyacityfc.com mapema leo kocha msaidizi wa City, Mohamed Kijuso amesema kulikuwa na makosa mengi kwenye mchezo uliopita jambo lililosababisha kupoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 2-0.
"Tumeanza mazoezi leo, tunataka kurekebisha makosa yote yaliyoonekana kwenye mchezo uliopita, yalikuwepo na ndiyo yalisababisha tufanye vibaya,ni lazima kuyaondoa ili tuwe vizuri kabla ya mchezo wa jumamosi dhidi ya JKT Ruvu ambao ni wazi tunatakiwaa kushinda ili tuwe kwenye mazingira mazuri katika msimamo wa ligi.
0 comments:
Post a Comment