Tuesday, August 11, 2015

Baada ya mapumziko ya siku tatu, Wekundu wa Msimbazi Simba kesho jioni wanatarajia kuanza mazoezi ikiwa ni muendelezo wa kujiwinda na michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara inayotarajia kuanza Septemba 12 mwaka huu.
Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Haji Sunday Manara amesema kikosi  chao kipo sawasawa kuanza matizi, ingawa mpaka muda huu hajui watatumia uwanja upi.

“Kesho jioni tunaanza mazoezi, sijajua ni uwanja gani, lakini nitakufahamisha baadaye”. Amesema Manara.

Agosti 8 mwaka huu ambayo ni siku ya Simba,  vijana wa Muingereza, Dylan Kerr walishinda 1-0 dhidi ya Sports Club Villa ya Uganda katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Goli pekee la ushindi lilifungwa na Awadh Issa Juma dakika ya 90 ya mchezo.

Mnyama Simba hajawahi kutwaa ubingwa tangu alipofanya hivyo msimu wa 2011/2012 na kuelekea msimu mpya wa 2015/2016, benchi la ufundi, viongozi, wachezaji, wanachama na mashabiki wake wana matumaini ya kurejesha heshima.


Hata hivyo, watakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa mabingwa wa kandanda Tanzania bara, Dar Young Africans na miamba ya kandanda Afrika Mashariki na kati, Azam FC ambao toka msimu wa 2012/2013 wanachuana nafasi mbili za juu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video