Simba imeanza mazoezi rasmi leo kujitayarisha na mchezo mwingine wa kimatifa wa kirafiki dhidi ya klabu ya URA ya nchini Uganda utakaopigwa Jumamosi (Agosti 15 mwaka huu) uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Mazoezi hayo yamefanyika kwenye uwanja wa Polisi Kilwa road.
Pia wanajiwinda na msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza Septemba 12 mwaka huu.
Toka watwae ubingwa wa bara msimu wa 2011/2012 chini ya kocha Milovan Circovic kutoka Serbia, Simba wanainusa harufu tu ya kombe hilo kutoka kwa mahasimu wao, Young Africans na Azam FC.

0 comments:
Post a Comment