Thursday, August 13, 2015

Uhusiano wa Eva Carneiro na Jose Mourinho umeingia dosari baada ya kocha huyo Mreno kumuondoa katika idara ya tiba itakayokuwa inasafiri na timu katika michezo mbalimbali na hata pia mazoezini.
Mourinho aliikosoa hadharani idara takje ya tiba baada ya sare ya mabao 2-2 dhdi ya Swansea City, kutokana na kwenda kumtibu Hazard, hali ya kuwa Mourinho anadai kiungo huyo alikuwa hajapata maumvivu yoyote, huku timu yake ikizidi kubaki pungufu, baada ya mlinda mlango wake Thibaut Courtois kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Lakini kumbukumbu ziandai kuwa hii si mara ya kwanza kwa Mourinho kufanya tukio hili.
Eva Carneiro akirushiana maneno na Jose Mourinho 

Februari 2005: Daktari wa Chelsea Neil Frazer aliondoka.
Ukiwa ni mwezi mmoja tangu Mourinho ajiunge na Chelsea kwa mara ya kwanza akaanza mzozo na timu yake ya madaktari baada ya kusababisha winga wake wakati huo Arjen Robben kukumbwa na majeraha ya mara kwa mara
Neil Frazer aliamua kuondoka wiki kadhaa kabla ya pambano la fainali ya kombe la Carling dhidi Liverpool baada ya kutoa taarifa kuwa Robben angekuwepo katika mchezo dhidi ya Cardiff huku winga huyo akiwa ametoka kuvunjika mguu takaribani wiki tatu nyuma.
Kutokana na taarifa hiyo, inasemekana Daktari huyo alitimuliwa siku chache baada ya tukio hilo, ingawa Chelsea walikanusha na kusema kuwa, ameamua kuondoka kutokana na matatizo ya kiafya yaliyokuwa yakimsumbua.
Arjen Robben akiwa chini kuugulia jereha lake la mguu.


October 2006: Jeraha la kichwa la Petr Cech dhidi ya Reading
Mourinho alitoa kauli hii: 'Endapo kipa wangu atakufa katika vyumba vya kubadilishia nguo aku akiwa njiani kuelekea hospitali Chama cha Mpira cha Uingereza lazima wafikiri mara mbili mbili'.



Novemba 2014: Mourinho amjia juu Sergio Ramos 
Hii ilikuwa ni baada ya Sergio Ramos kutilia shaka uamuzi wa Mourinho kukataa kuwaruhusu Diego Costa na Cesc Fabregas kujiunga na timu yao ya taifa.
Mourinho akasema hivi;'Tangu nimemfahamu Sergio Ramos amekuwa ni mchezaji wa aina ya kipekee sana, lakini sio daktari,' alisema. 'Sio yeye wala mimi ambaye ni daktari. Nafanya kila liwezekanalo ila mimi sio daktari.
Lakini cha kushangaza Costa alicheza mchezo dhidi ya West Brow ilhali ilisemekana kuwa ni mgonjwa.



May 2015: Chelsea walikosolewa dhdi ya jeraha la kichwa la Oscar.
Hii ilitokan na wataalamu kusema kuwa haikuwa sahihi Oscar kurudi uwanjani baada ya kugongana na kipa wa Arsenal David Ospina lakini, Mourinho kwa upande wake akasema kuwa Oscar hakuwa na maumivu yoyote hivyo yalikuwa yakiongelewa yoyote yalikuwa ni uongo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video