Monday, July 20, 2015

Kocha Jose Mourinho wa Chelsea wiki hii ameonekana sana kutetea uamuzi wake wa kumsajili mshambuliaji na nahodha wa Colombia, Radamel Falcao Garcia.
Akionekana kujipa moyo kutokana na kutofanya vizuri kwa mshambuliaji huyo msimu uliopita akiwa Old Trafford, Mourinho anadai Falcao hana tatizo tena la majeruhi.

Mourinho alienda mbali na kusema, kama Falcao angekuwa bado hajapona, wasingepoteza pesa kumsajili ingawa ni kwa mkopo.

Hata hivyo kocha huyo ametoboa siri ya kilichosababisha usajili wa mshambuliaji huyo ukamilike. 
Mourinho anasema aliomba ushauri kutoka kwa walinzi wake John Terry pamoja na Gary Cahil.

Jose anasema kuwa, Cahil na Terry walimshauri kwamba hata walipokutana na mchezaji huyo, bado alikuwa na 'movements' za hatari na kwamba anaweza kufunga magoli mengi akipewa nafasi.

Mourinho amekaririwa mara kadhaa akisema, anasikitika kuona kuwa watu wanafikiri kwamba Falcao yule wa Manchester United ndiye halisi. Jose anasema katika makali yake Falcao hana mfano wake.


Wote tunasubiri kuona kamali hii ya Mourinho kama itazaa matunda msimu huu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video