Kikosi cha Azam FC kinachojiandaa na mashindano ya Kagame Cup kimeendelea na maandalizi yake kwenye viunga vya Azam Complex huku benchi jipya la ufundi likifurahia vipaji vilivyopo.
Wasaidizi wa Stewart toka uingereza na Romania wameonekana kufurahishwa sana na nidhamu, vipaji na kujituma kwa wachezaji waliowakuta Azam FC na wakasema watahakikisha wanatumia maarifa yao yote kuhakikisha wanaifanya Azam FC klabu inayoheshmika Afrika.
Wachezaji wa kigeni wameongezea utamu wa mazoezi hayo ambayo wiki iliyopita yalitawaliwa na wachezaji wa kikosi cha vijana (Under 20)
Azam FC imekuwa ikifanya mazoezi ya kujenga mwili zaidi kwa kukimbia, Gym, Kuogelea na kuchezea mpira.
0 comments:
Post a Comment