Friday, May 1, 2015

ETOILE du Sahel wanaikaribisha Yanga katika mechi ya marudiano ya hatua ya 16 bora ya kombe la Shirikisho inayopigwa kesho mjini Sousse Tunisia kuanzia saa 3:00 usiku kwa saa za Tanzania.
Mabingwa wa Tanzania, Yanga, wanahitaji ushindi wa aina yoyote ile au sare ya angalau magoli 2-2 ili kusonga mbele moja kwa moja. Hii inatokana na sare ya 1-1 waliyopata uwanja wa Taifa, Dar es salaam majuma mawili yaliyopita.
Kuelekea katika mechi hiyo, MPENJA BLOG imezungumza na mchezaji wa zamani wa Yanga ambaye kwa sasa ni kocha wa mpira wa miguu na mchambuzi wa soka katika kituo cha Azam TV, Ally Mayay Tembele akieleza mbinu ambazo Yanga wanatakiwa kutumia ili kuwashinda Etoile.
Mayay ameanza kwa kufafanua kuwa mpango wa mechi (Game Plan) huanzia nje ya uwanja na unapoingia uwanjani unakwenda kutekeleza tu.
“kwanza kwa nje ya uwanja nafasi kubwa ni saikolojia, kama timu unajiandaa na kufanyiwa vibaya ‘Fitina’ kuanzia hotelini, unapoingia uwanjani na sehemu yoyote ile”. Amesema Mayay na kusisitiza: “ Mazingira hayawezi kuwa rafiki, ukiona mtu anakutendea vibaya unatakiwa kujiandaa kufunga, unajua kabisa kwamba kesho mimi nitafunga, kwa mfano walikaa karibia saa tatu uwanja wa ndege, sio suala la kulalamika, ni suala la kujiandaa”
Beki huyo na kiungo wa zamani wa Yanga ameeleza mbinu za uwanjani ambazo Wanajangwani wanatakiwa kuzitumia ili kuwamaliza Waarabu.
“Ukifika uwanjani kwenye mechi kubwa kama hiyo unatakiwa kujiandaa kucheza mpira, ukisema unakwenda kukaba utapata matatizo, siku zote ukiwaruhusu wao wacheze mpira maana yake watakushambulia muda wote na ukishambuliwa kwa muda mrefu uwezekano wa kufanya makosa ni mkubwa, kwahiyo utafungwa tu”
YANGA WAFANYEJE SASA?
Mayay anasema: “Kikubwa ni kuhakikisha wanamiliki mpira, uliona katika mechi ya kwanza hapa nyumbani, kipindi cha kwanza waliwaruhusu Waarabu watengeneze nafasi nyingi sana ingawa hawakuwa makini sana wale Etoile du Sahel, kama wangekuwa makini wangepata mabao matatu”
“Yanga wategemea kuwa watashambuliwa kutoka dakika ya kwanza mpaka ya mwisho, njia sahihi ya kujilinda ni kukaa na mpira, angalau umiliki uwe asilimia 50 kwa 50, usiache wamiliki mpira wao kwasababu utakuwa unakaba muda wote”.
KIUNGO FUNDI HARUNA NIYONZIMA HAYUPO KWENYE MECHI HIYO KUTOKANA NA KADI TATU ZA NJANO, JE ITAATHIRI TIMU?
Mayay anajibu: “Haruna (Niyonzima) hatakuwepo leo, ni mchezaji ambaye ana umuhimu pale timu inapotaka kucheza mpira, sio mtu muoga, kuna wakati mechi inakuwa ngumu na viungo wanashindwa kucheza kwa mfano akikaa na mpira mara ya kwanza akaharibu hataki kwenda kuomba, lakini Haruna ni mtu anayefanya kazi, lazima kutakuwa na pengo”
“Yanga wana watu wanaoweza kuifanya kazi nzuri, wanaweza wasiwe wabunifu sana kama Haruna kwasababu anakaa na mpira na anasaidia kiungo, Telela (Salum) hayuko fiti kwasababau hajacheza, lakini kutokana na uzoefu wake wa kucheza Yanga na baadhi ya mechi za kimataifa anaweza kucheza vizuri ingawa si kwa kiwango cha juu”.
NANI MWINGINE ANAWEZA KUFANYA KAZI NZURI SAFU YA KIUNGO?
Mayay anafafanua: “Wapo baadhi ya watu kama Said Juma, kama atapewa nafasi anaweza kucheza mpira, inawezekana katikati pasiwe na ubunifu, lakini kikubwa ni kumiliki mpira, mwalimu anaweza kuweka washambuliaji watatu, Kpah Sherman, Mrisho Ngassa pamoja na Msuva au hata Tegete, Mrwanda ambao wamekwenda. Katikati kuna akina Makapu (Said Juma), Telela (Salum), Mbuyu (Twite) au hata Zahir (Rajab) akacheza kama kiungo mkabaji na wakaongeza nguvu kwasababu katikati licha ya kuhitaji ubunifu pia panahitaji nguvu”.

Kila la kheru Yanga katika mechi yenu!!

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video