Uongozi wa Simba umeonyesha umepania kuimarisha safu yake ya ulinzi baada ya kumnasa beki wa JKT, Mohammed Fakhi, jana usiku.
Faki amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha.
“Kweli Faki amesaini miaka miwili, hii ni sehemu ya kuhakikisha tunaimarisha safu ya ulinzi,” Hans Poppe alikaririwa na Salehjembe.
Faki aliichezea JKT kwa ufanisi mkubwa katika msimu uliopita.
0 comments:
Post a Comment