Sunday, May 3, 2015

HATIMA ya nafasi ya pili msimu huu huenda ikajulikana leo wakati Simba inatarajia kuikaribisha Azam fc katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara itayopigwa leo jioni uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Azam wapo nafasi ya pili kwa pointi 45 baada ya kucheza mechi 23, wakati Simba wanashika nafasi ya nne wakijikusanyia pointi 41 kufuatia kushuka dimbani mara 24.
Kama Simba wanahitaji kuchukua nafasi ya pili wanahitaji kushinda mechi ya leo ili kufikisha pointi 44 wakisubiri mechi ya mwisho dhidi ya JKT Ruvu Mei 9 mwaka huu na wakiiombea Azam itoe sare moja na kufungwa mechi moja.
Baada ya mechi ya leo, jumatano ijayo Azam wanacheza na Yanga uwanja wa Taifa na watamaliza ligi mei 9 mwaka huu dhidi ya Mgambo JKT uwanja wa Azam Complex.
Kama Azam watafungwa na Simba halafu wakafungwa na Yanga, maana yake wataendelea kuwa na pointi 45, Simba 44. Mechi ya mwisho wakishinda dhidi ya Mgambo, Simba hatakuwa na chake, matokeo pekee yatakayowasaidia Simba ni kuona Azam anatoka sare na Mgambo baada ya kufungwa mechi mbili.
Kama matokeo hayo yatatokea maana yake Azam atafikisha pointi 46 ambazo Simba watazivuka kama watashinda tena mechi ya mwisho dhidi ya JKT Ruvu .
Hivi ni hesabu za nje ya uwanjani, matokea ya mpira wa miguu hupatikana uwanjani.
Kuelekea mechi ya leo, Simba kupitia kwa afisa habari wake, Hajji Manara wamesema wanaichukulia kwa uzito wa hali ya juu kuhakikisha wanavuna pointi tatu.

“Kila mtu anajua umhimu wa mechi hii, tunaichukulia kwa uzito mkubwa, mechi  ni kubwa, tunacheza na timu nzuri, tumejipanga kuhakikisha tunashinda. Hakuna mechi rahisi, hata wateja wetu Yanga inakuwa mechi ngumu lakini mwisho wa siku tunawafunga”. Amesema Hajji.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video