Saturday, May 9, 2015

Na Mwandishi Wetu
MPAMBANO mkali wa masumbwi utafanyika Bagamoyo Mei 16 katika ukumbi wa  che kwa che uliopo Bagamoyo mjini, mpambano huo utawakutanisha bondia Iddi Pialali wa Kiwangwa Bagamoyo atakaezipiga na Adam Ngange wa Chanika Dar es salaam.
Mpambano huo utachezwa baada ya kila bondia kujigamba kuwa yeye ni zaidi ya mwenzie, siku hiyo pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali wenye upinzani mkali katika masumbwi,
Rashidi Haruna atakumbana na Kaminja Ramadhani na Harid Hongo atakabiliana na Kishoki Mbishi, mpambano mwingine ni Abdallah Samata atakaye zidunda na Maono Alli 
Mipambano hiyo inaletwa kwenu na Sharif Promotion wakati mgeni rasmi siku hiyo ni bondia kutoka Morogoro Cosmas Cheka, ambaye atakuja kuwapa nasaha mbalimbali mabondia na mashabiki wa mchezo wa masumbwi kuweza kusonga mbele kwa mchezo huo mjini Bagamoyo,
kingilia katika mpambano huo ni Tsh, 8000 kwa V.I.P na kwaida ni sh. 5000.
Katika mpambano wa siku hiyo, kutakuwa na upatikanaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar vs Manny Pacquaio 2015 , Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi.
Pia kutakuwa na vifaa vya mchezo vitakavyokuwa vikigawiwa na kocha  Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa gharama nafuu na kocha huyo kwa ajili ya kuhamasisha mchezo wa masumbwi nchini.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video