Thursday, May 28, 2015


Perez (kulia) amemfukuza Carlo Ancelotti

Wachezaji wake wametoa madukuduku yao. Wanataka Carlo aendelee kuwafundisha. Vivyo hivyo kwa mashabiki, kupitia vyombo vya habari jijini Madrid, walisema wanataka aendelee kuwepo. Watu wa Bernabeu wamekuwa waaminifu, mara chache sana wamekuwa waaminifu hivi linapokuja suala hili. Wanapenda wawe naye tena msimu ujao. Yeye (Ancelotti) pia hapendi kuondoka.

Sasa ni kwa nini Ancelotti si kocha wa Real Madrid tena?

 Hili ni swali ambalo halina utani hata kidogo. Unapoulizwa swali kama hili, wengine wanaweza kusema ni kwa sababu ya Barcelona. Baada ya ‘kutoka kapa’ msimu huu.  Sio tu kwamba Barcelona wameshinda La Liga, huku kukiwa na uwezekano wakushinda makombe matatu msimu huu – lakini pia wamekuwa gumzo tena kwa watu wapenda soka kutokana na jinsi wanavyotandaza soka la uhakika.

Hiyo ni kitu hatari kwa kocha yeyote atakayechaguliwa na Rais wa Madrid kukutana nayo. Unaweza kuwa ulihisi hili, Florentino asingeweza kukubali hali hii. Sio kwamba, Perez anataka Real ishinde makombe makubwa tu lakini pia anataka timu yake iwe tishio balaa kama ilivyokuwa kipindi akiwa kijana mdogo.

Kipindi cha kina Alfredo Di Stefano, Ferenc Puskas, Francisco Gento na Jose Santamaria. Kipindi ambacho watu walikuwa wakiwaangalia wanaume kumi na moja wakiwa kwenye jezi zao nyeupe, wakiwafanyia ‘maangamizi ya kutisha’ timu pinzani, sio tu kuwa na mafanikio na klabu kutisha sokoni. Perez anataka Real Madrid itawale kila mahali lakini utawala uanzie uwanjani.

Kwa hiyo Barcelona inaposhinda makombe. Ni kitu kibaya. Lakini Barca ilipomchukua Neymar kabla yake (kitu ambacho hadi leo bado kinamuumiza), ni jambo lingine baya. Lakini yote hayo tisa, linapokuja suala la Lionel Messi, Neymar, na Suarez kuwa ni utatu unaotisha zaidi duniani basi hapo Perez anazidi ‘kuvurugwa’.

Hebu tuyaweke hayo yote katika upande mmoja kwa muda.

Ni kweli Ancelotti ameondolewa kwa sababu timu yake ilishinda makombe manne tu katika misimu miwili? Inawezekana. Kushinda La Liga au Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya sio tiketi ya moja kwa moja kuendelea kuwa kocha wa Real. Muulize Jupp Heynckes, muulize Vicente Del Bosque: watu waliotemwa na Perez lakini wakaja kutisha sana baada ya kuondoka.

Kikosi cha Ancelotti kilitakiwa kiwe angalau kimeshinda La Liga mara moja, au mara zote mbili wakati akikiongoza. Lakini tujikumbushe jinsi alivyoshinda makombe yake manne. Barcelona ilifungwa kwenye fainali ya Kombe la Mfalme. Atletico huku wakidhani wameshashinda Ligi ya Mabingwa, ghafla walijikuta wakishushiwa ‘mvua’ ya magoli kwenye mechi ya fainali.

Ushindi wa 2-1 kwenye Super Cup ya Ulaya ambayo huwa ni mechi moja tu, waliifunga Sevilla. Kilikuwa ni kisasi kizuri kwa sababu Sevilla waliwaharibia kampeni yao ya kushinda La Liga.

Je waliifunga moja ya timu kubwa wakati wanashinda Kombe la Dunia kwa Vilabu? Hapana. Lakini kuwa bingwa wa dunia inatia moyo sana na inawafanya wachezaji wawe vema kisaikolojia.

Kwa makombe hayo aliyoyashinda, je alijua ni lazima ashinde La Liga au kibarua chake kitaota nyasi?

Napenda kujua jibu lake, lakini nadhani jibu ni hapana. Kusema kwamba kushinda taji hilo kungemfanya awe salama moja kwa moja.

Kushinda tena Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya ingekuwa ni jambo la kihistoria. Haijawahi kufanyika kabla (kwa utaratibu huu wa sasa).  Lakini ni ubabe uliopitiliza kusema kwa kocha aliye katika msimu wake wa pili, afanye jambo ambalo hakuna aliyeweza kulifanya kabla au anafukuzwa.

Kwa hiyo wakati Ancelotti akielekea kwenye mwaka wake wa sabato (sabbatical year – hii ni kulingana na alivyosema mwenyewe). Je ni taji la La Liga ndilo lililomgharimu? Inawezekana kabisa.

Hakuna kipindi ambacho tungeweza kusema kwamba Real Madrid imeshashinda La Liga lakini kuna kipindi ilionekana kuwa na nguvu sana. Kusema kweli ilijichanganya yenyewe na kuliachia kombe hili, ndio maana Barcelona – nayo ambayo kuna kipindi hali ya ndani ya klabu haikua shwari – iliweza kurudi kwenye kampeni na kushinda.

Kipindi ambacho Ancelotti aliadhibiwa zaidi ni kile kipindi kilichozidi mwezi kati ya siku za mwanzoni za mwezi Februari hadi katikati ya mwezi Machi. Kipindi hiki kilikuwa kibaya zaidi kwa zama za hivi karibuni za klabu hiyo.

Vipigo – ‘dhahama’ iliyowashukia Calderon – kutoka kwa Atletico, Athletic, Barcelona na Schalke, droo ya nyumbani dhidi ya Villareal. Hali ya kujiamini ilipotea na kulikuwa hamna njia sahihi (kutosha) ya kutatua matatizo yaliyokuwa yanawakabili.

Hicho ndicho kipindi ambacho Madrid walipoteza taji hilo na Ancelotti kupoteza kazi yake.

Kama Real wangepata sare dhidi ya Atleti na Athletic, na kuifunga Barcelona (ambayo walionekana wanaweza katika kipindi cha kwanza pale Camp Nou) na kupata pointi zote tatu dhid ya Villareal. Wangekuwa mabingwa sasa hivi. Hata sare tatu za ugenini na ushindi nyumbani bado ingeweza kuwapa ubingwa.

Makosa tena yalionekana kwenye mechi dhidi ya Juventus, hasahasa kushindwa kupata ushindi kwenye mechi ya pili.  Madrid haikuwa na nguvu, fiti, makini, haikuweza kushambulia na pia ilikosa stamina. Walianza kuonekana kama Barca ilivyokuwa msimu uliopita.

Tatizo lingine kubwa ilikuwa hali ya kujirudia rudia ya majeruhi kwa wachezaji. Chanzo kinaweza kuwa mipango yao ya uimara kwa wchezaji (fitness strategy) inakosa baadhi ya vitu au mazoezi yao ya kila siku hayafanywi kwa usahihi.

Lakini – hapa ndipo boss Perez anatakiwa kuwa makini zaidi – Barcelona wameonesha msimu huu kwamba hilo linaweza kusahihishwa. Mchanganyiko wa Ubora namaandalizi sahihi ya mazoezi, mzunguko (rotation) bora wa wachezaji wa kiwango cha juu.

Madrid inabidi iangalie nini kimewazunguka. Wameshinda kombe moja la La Liga katika misimu saba iliyopita, wameshinda makombe mawili ya Ligi ya Mabingwa, mataji matatu ya La Liga na mawili ya Kombe la Mfalme katika miaka 12 ya Perez kama Rais wao. Wanadhihakiwa kwa hayo pia.

Kama wakiangalia pembeni yao – sio tu kwa Barcelona bali Sevilla na Atletico pia – kwa nini Perez hajifunzi kuwa, njia ya kuelekea mafanikio na makombe zaidi ni aidha kuwa na kanuni moja inayoendana na DNA ya klabu au kumweka mtu mmoja, awe kocha kwa kipindi kirefu (kama Monchi kwa Sevilla) ili kuhakikisha kwamba mawimbi hayasababishi Meli kuzama hata pale hali ya hewa inapobadilika.

Atletico wao wameweza kushinda makombe mawili ya Ligi ya Europa, moja la Mfalme na moja la La Liga katika misimu mitano iliyopita. Hayo ni matunda yaliyotokana na mmiliki wao, Miguel Angel Gil, ambaye anawaamini wakurugenzi bora wa mpira, wamwongoze. Ataandika kile anachokitaka, aina ya mpira ambao wadhamini na mashabiki watalipa ili kuungalia, pia atapanga ukomo wa bajeti.

Sevilla imekuwa ni klabu inayojiendesha yenyewe tangu mwaka 2000, ya Ramon “Monchi” Rodriguez. Ameitengenezea klabu hela nyingi na kuendeleza mfumo mzuri wa  kuendeleza vijana, na ushindi wa Sevilla kwenye Ligi ya Europa (Europa League) jana usiku kunamaanisha hilo limekuwa kombe lao kubwa la sita katika miaka tisa (bila kuhesabu Super cup za Spain). Kuwa makini Florentino.

Na hatimaye, Barcelona. Mafanikio yao yametokana na Johan Cruyff aliyeona amedharauliwa kuuzwa Real Madrid bila ruhusa yake mwaka 1973, na kulazimisha kuuzwa Camp Nou, badala yake. Baada ya kurudi kwake kwa mara ya pili kwenye klabu (kama kocha) tangu 1989 mpaka sasa klabu imeweza kufikia maono yake, kwa kufanya miaka 25 iliyopita kuwa miaka yao yenye mafanikio na kuvutia zaidi katika historia. Hii ndio klabu inayomnyima usingizi Florentino, lakini bado hajifunzi kwao.

Carlo Ancelotti angesikilizwa ili atoe mwongozo wa nani asajiliwe nani aachwe atemwe, na nani auzwe.


Lakini je kumuondoa Ancelotti kutaponya matatizo ya Real Madrid? Hapana. Kwa sababu tatizo kubwa la Real Madrid, hata pale mambo yanapokuwa mazuri, linabaki kuwa moja tu, nalo ni Florentino Perez. Yeye ni maji na petroli kwenye tanki lao la mafuta.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video