Tuesday, May 5, 2015

MSHAMBULIAJI hatari, Emmanuel Anord Okwi, raia wa Uganda, ameendelea kuguswa na sapoti kubwa anayopewa na wachezaji, viongozi, benchi la ufundi na mashabiki wa klabu ya Simba.
Okwi amekuwa akibanwa sana na mabeki wa timu pinzani kwasasa kutokana na kutotabirika akiwa uwanjani na ni vigumu kujua atafunga muda gani kwani ni mbunifu na mjanja wa kupiga mashuti ya kushitukiza.
Makipa kadhaa wakiwemo Mwadini Ali wa Azam na Ally Mustafa wa Yanga wameshaonja joto la jiwe kutokana na magoli ya uwezo binafsi ya Okwi walipokutana katika mechi za ligi kuu ambapo Simba ilitoka sare ya 1-1 na Azam na machi 8 mwaka huu walishinda 1-0 dhidi ya Yanga.
Baada ya mechi ya  mwishoni mwa juma hili dhidi ya Azam fc ambapo Simba walishinda 2-1, Okwi alisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Simba nje ya mlango wa ndani wa kuingilia uwanjani.
Okwi (kushoto) akijaribu kuchuana na Aggrey Morris wa Azam juzi uwanja wa Taifa

Nyota huyo alikuwa wa mwisho mwisho kutoka katika vyumba vya kubadilishia nguo akifuatana na Waganda wenzake, Joseph Owino, Juuko Mursheed, Simon Sserunkuma na Danny Sserunkuma.
Walipofika nje walikuta kuna umati wa mashabiki ilipopaki basi ya Simba, yeye na wenzake wakaamua kupita njia nyingine, wakati anajaribu kufanya hivyo kuna jamaa mmoja (jina halikufahamika kwa haraka) alimfuata Okwi na kumwambia unaona watu wale! Wapo pale kwa ajili yako, nenda kawasalimie.
Wachezaji wenzake wakamkataza, lakini Okwi akaona ni busara kwenda kuwatimizia haja yao, akatoa simu, wallet yake na kumkabidhi Owino na kwenda kuwasalimia.
Baada ya kufika pale walimshangilia mno na kumkumbatia wakionesha kuridhishwa na uchezaji wa ‘mfalme’ huyo wa Msimbazi.
Mtandao huu ukamuuliza Okwi anajisikiaje kupendwa kiasi hicho, naye akajibu;
“Kwanza Simba ni nyumbani, hii ni sehemu ninayoishi kwa furaha, licha ya changamoto ninazopata nikiwa uwanjani (kukamiwa na mabeki), bado Wanasimba wamekuwa nami muda wote, hali hii inanifanya nijitume mazoezini ili niendelee kufanya vizuri”.
“Makocha wangu, mashabiki wote, wachezaji wamekuwa upande wangu, nina furaha mno ndani ya klabu hii iliyonipa heshima kubwa. Nawapenda Wanasimba wote”.

Mpaka sasa Okwi amefunga magoli 11, mabao 6 nyuma ya kinara Simon Msuva.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video