Thursday, April 30, 2015

YANGA SC imetua salama nchini Tunisia na msafara umeshawasili mjini Sousse ambapo mechi ya marudiano ya hatua ya 16 dhidi ya Etoile du Sahel itapigwa kesho kutwa jumamosi kuanzia saa 3:00 kwa saa za Tunisia.
Kocha mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm anakiongoza kikosi chake katika mazoezi kuanzia saa 11:00 jioni kwa saa za Tunisia , kwa saa za Tanzania ni saa 1:00 usiku.

Tunisia wapo nyuma kwa saa mbili ukilinganisha na saa za Afrika mashariki.
Pluijm amesema kurejea kwa Salum Telela, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kutaimarisha timu yake katika mchezo huo muhimu.

Hata hivyo imeripotiwa kwamba Yanga walicheleweshwa kwa zaidi ya saa mbili uwanja wa Ndege baada ya kuwasili mchana na wenyeji wao Etoile walichelewe kufika na kuwapa usafiri, lakini wachezaji, viongozi na wadau wote walioko huko wako vizuri na wamejiandaa kwa fitina zote.
Etoile waliwapatia basi Yanga lililowasafirisha kutoka mjini Tunis kwenda Sousse kiliometa 140 kutoka mji mkuu Tunis.
Mechi ya kwanza iliyopigwa uwanja wa Taifa Dar es salaam takribani majuma mawili yaliyopita, timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
Yanga wanahitaji ushindi au  sare ya zaidi ya magoli 2-2  ili kusonga mbele moja kwa moja.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video