MECHI ya watani wa jadi ligi kuu England, Manchester United dhidi ya Manchester City inaanz amajira ya saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika mashari.
Mechi hiyo inapigwa uwanja wa Old Trafford, Mtandao huu unakuleta takwimu na taarifa za kweli kuhusu mechi.
Manchester United imepoteza mechi nne zilizopita dhidi ya Manchester City, lakini hawajawi kupoteza tano.
Sergio Aguero amefunga magoli manne katika mechi tatu zilizopita dhidi ya Manchester United.
Mashetani wekundu wamefungwa magoli 11 katika mechi tatu za ligi walizocheza Old Trafford dhidi ya Manchester City.
Magoli yote ya Edin Dzeko katika mechi za ligi aliyofunga dhidi ya Man United alifunga Old Trafford.
Magoli matatu ya Wayne Rooney kati ya 8 aliyofunga dhidi ya Manchester City alifungwa nje ya Trafford.
Manchester City inaweza kuwa timu ya kwanza ya ligi kuu England kuandika rekodi ya kushinda mara tano mfululizo dhidi ya Manchester United.
Hakuna kocha yeyote wa Manchester City aliyepoteza mechi nne mfululizo tangu Stuart Pearce septemba 2006.
HABARI ZA TIMU ZOTE
MAN UNITED
Robin van Persie hataichezea Manchester United leo hii licha ya kurudi katika mazoezi ya timu ya kwanza tangu alipoumia kifundo cha mguu februari 21 mwaka huu dhidi ya Swansea City.
John Evans amefungiw, Luke Shaw anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja, Chriss Smalling anaumwa, kiungo Andreas Pereira yupo na kikosi cha U-20 cha Brazil.
MAN CITY
Nahodha wa City, Vicent Kompany ana wasiwasi kucheza mechi ya leo kutokana na maumivu ya nyama za paja.
Kompany alibanwa na misuli katika kipigo cha 2-1 walichopata jumatatu kutoka kwa Crystal Palace.
Mshambuliaji Wilfried Bony na Stevan Jovetic wana majeruhi ya vifundo vya mguu,
Mlinzi Dedryck Boyata ana majeruhi ya goti


0 comments:
Post a Comment