SIMBA SC imerejea jijini Dar es salaam kujiandaa
na mechi dhidi ya Mbeya City fc ikitokea kanda ya ziwa ilipocheza mechi na
Kagera Sugar ikishinda 2-1 na kushiriki shughuli za kijamii Rorya- Mara na
Mwanza.
Mbeya City fc na Simba zitapepetana aprili 18
mwaka huu uwanja wa Sokoine Mbeya.
Watani zao wa jadi , Young Africans jana
walishinda 3-1 dhidi ya Mbeya City fc na kuendelea kujikita kileleni mwa ligi
kuu wakikusanya pointi 46 baada ya kucheza mechi 21 wakifuatiwa na Azam fc waliocheza
mechi 20 na kukusanya mzigo wa pointi 38
Kituo cha redio cha E FM kilimtafuta msemaji wa
Simba Hajji Sunday Manara na kumhoji habari za Simba na hatimaye kumchokoza kwa
kumuuliza matokeo ya Yanga.
Mtangazaji wa kituo hicho, Maulid Kitenge ndiye
alifanya mahojiano hayo kwa njia ya Simu ambapo Hajji alikuwa anaangalia mechi
ya Manchester United dhidi ya Manchester City.
Hajji ni shabiki wa kutupwa wa Simba na Man United
na mahojiano yalienda hivi;
Mtangazaji: Leo hii mmesikia Young Africans
wakizidi kujikita kileleni?
Hajji: Nani?
Mtangazaji: Young Africans?
Hajji. Eheeeh!
Mtangazaji:Wamezidi kujikita kileleni baada ya
kumnyoa Mbeya City
Hajji: Alaaah! Mimi naangalia United na City
hapa,hiyo ndo unaniambia wewe
Mtangazaji: Huna taarifa hizo?
Hajji: Naishughulikia Simba, mimi naishughulikia
Simba na United
Mtangazaji: Huna taarifa za Yanga?
Hajji: Yanga inanihusu nini? Kwani lazima uniulize
mimi, si umuulize msemaji wao au viongozi wao, kwani hawana?
Mtangazaji: Kasi yao ya ligi huioni? Wao ndio vinara
Hajji: Kasi yao maana yake nini,sisi tunashughulikia mechi
zetu, wewe umeuliza habari za Simba nimekujibu, sasa unaniuliza habari za Yanga
zinanihusu nini?
Mtangazaji: sasa kasi yao ninyi haiwatishi?
Hajji: Tunamuogopa nani, angalia huku goli la tatu
wewe! la United
Mtangazaji: Kwahiyo wewe huna shughuli kabisa na
Young Africans?
Hajji: Nilikuwa naangali jinsi ilivyopigwa na
Antonio Valencia, Yanga sina shughuli nao.
Mtangazaji: Unawaambia nini sasa Yanga?
Hajji: Niwaambie nini?, mimi ni kiongozi wa Simba
na si kiongozi wa Yanga, unaniuliza ya Yanga inanisaidia nini, mimi kiongozi wa
Simba, nalipwa na Simba, sina habari za Yanga, unataka kuniingiza sokomoko
bwana kila wakati unaniuliza habari za Yanga.


0 comments:
Post a Comment