Monday, April 13, 2015


Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam
KOCHA bora msimu uliopita, Juma Mwambusi wa Mbeya City fc amefungwa mechi ya tatu kati ya nne alizokutana na Yanga katika misimu miwili mfululizo waliyoshiriki ligi kuu Tanzania bara tangu wapande mwaka jana.

Hii inatokana na kipigo cha 3-1 walichopata jana uwanja wa Taifa dhidi ya Yanga, huku wakiwa pungufu kwa dakika 37’ za mchezo kutokana na Themi Ferlix kuoneshwa kadi nyekundu na muamuzi Mathew Akrama baada ya kumchezea rafu mbaya Salum Telela ambaye baadaye dakika ya 61 alishindwa kuendelea na mchezo.

Mechi mbili za msimu uliopita, Mbeya City ilitoka sare ya 1-1 na Yanga uwanja wa nyumbani wa Sokoine kabla ya kufungwa 1-0 uwanja wa Taifa.

Msimu huu mechi ya kwanza walifungwa 3-1 uwanja wa Sokoine na jana wamefungwa kipigo kama hicho uwanja wa Taifa.

KOCHA MWAMBUSI ANASEMAJE KUHUSU KIPIGO HICHO?

Juma Mwambusi

“Bahati mbaya sijasikitika kwa matokeo niliyopata kwasababu katika matokeo mengi nimekuwa nikifanikiwa, nilikuja uwanja wa Taifa na kushinda (2-1 dhidi ya Simba januari 28 mwaka huu). Sema ninasikitika tu kwasababu nimepoteza na nilikuwa nahitaji ushindi, mpira una matokeo matatu, ninachosema ni kwamba nimepambana. Mpaka tunakwenda mapumziko tulikuwa tumefungwa magoli 2-1 na tuliporudi kipindi cha pili wakaongeza goli la tatu dakika za mwanzo”


ANAIZUNGUMZIAJE KADI NYEKUNDU YA THEMI FELIX?


Mwambusi anasema: “Lakini tulichanganywa na kadi nyekundu ya muamuzi, ilikuwa na matatizo, basi tunakubali kuwa tumefungwa 3-1 na Yanga na tunajipanga kwenda kupambana na Simba Mbeya”


KUELEKEA MECHI YA SIMBA ANAWAAMBIA NINI MASHABIKI WA MBEYA CITY FC?


Mwambusi anajibu: “Wapenzi wa Mbeya City ambao wapo nchi nzima kwanza niwashukuru kwa kutuunga mkono kwa kiasi kikubwa, ninachosema mechi imeshaisha, tunayasahau na tunaenda kupambana na Simba kuhitaji pointi tatu pale nyumbani. kwahiyo waje watupokee kwa hamasa kubwa, wachezaji wamejipanga, watuombee tufike salama katika safari yetu ili tujiandae vizuri”


Mbeya City fc na Simba zitapambana jumamosi aprili 18 uwanja wa Sokoine Mbeya katika mfululizo wa ligi kuu soka Tanzania bara.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video