Timu ya
Mtwivila city ya mjini Iringa ipo kwenye
maandalizi makubwa kujiandaa na michezo ya kumtafuta bingwa wa mikoa ili iweze
kupanda ligi daraja la pili
Katika
kuhakikisha inafanya vizuri timu hiyo yenye maskani yake mtaa wa Mtwivila
hapa Iringa mjini, kwa sasa inafanya mazoezi yake katika viwanja vya chuo kikuu
kishiriki cha Mkwawa ambapo lengo kubwa la timu hiyo ni kupanda daraja msimu wa
2015-2016 utakaoanza baadaye mwaka huu.
Pamoja na hayo
lakini bado timu hiyo ya Mtwivila city ina ukata wa fedha na sasa wapenzi na
wadau wa soka wanaombwa kuichangia kwa hali na mali ili iweze kufanya vizuri
katika michuano hiyo ya ligi ya mabingwa wa mikoa inayotazamiwa kuanza kutimua
vumbi karibuni
Makamu
mwenyekiti wa timu hiyo, Ibrahim Tungo alisema
‘‘Naomba sana wadau na wapenzi wa soka mkoa wa
Iringa watusaidie katika mapambano yaliyo mbele yetu kwani tunatakiwa
kushiriki kikamilifu na hata tupande daraja pamoja, mafanikio ya Mtwivila city
ni mafanikio ya soka la Iringa tukiungana pamoja tutaweza kukidhi azma yetu ’’
Pamoja na
hayo, timu hiyo ambayo kwa sasa ni gumzo
kwa wakazi wa Manispaa ya Iringa imepata
nafasi ya kushiriki kwenye michuano ya kombe la MUUNGANO LA MUFINDI ambalo
linatazamiwa kuanza kutimua vumbi katika wilaya ya MUFINDI mapema mwezi wa tano
.
Timu ya
Mtwivila city yenye wachezaji wengi ambao bado wapo masomoni inatazamiwa kutoa
ushindani mkali katika michuano ambayo
itashiriki .


0 comments:
Post a Comment