Thursday, April 16, 2015

SIMBA SC wapo nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu wakijikusanyia pointi 35 baada ya kucheza mechi 21 sawa na Azam wenye pointi 39 nafasi ya pili.
Tofauti ya Simba na Azam ni kwamba Wanalambalamba wameshinda mechi nyingi zaidi ukilinganisha na Mnyama.

Azam wameshinda 10, sare 9 na kufungwa 2. Wamefunga magoli 27 na kufungwa 14, tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa ni 13.

Simba wao wameshinda mechi 9, sare 8 na kufungwa 4. Wamefungwa magoli 27 na kufungwa 15, tofauti ya magoli ni 12.

Mbeya City fc wapo nafasi ya 10 kwa pointi 25 baada ya kucheza mechi 22. Wameshinda mechi 5, sare 10 na kufungwa 7. Wamefunga magoli 17 na kufungwa 21, tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa ni -4.

Kwa jinsi msimamo ulivyo, kati ya Mbeya City na Simba, Mnyama hawezi kushuka daraja, lakini Mbeya City kama hawakazi lolote linaweza kutokea.

Timu tatu tu, Yanga, Azam, Simba ziko salama, lakini nyingine zote zinaweza kushuka daraja.

Timu ya 12 katika msimamo (JKT Ruvu) ina pointi 24 ikitofautiana na Mgambo JKT iliyopo nafasi ya tano kwa pointi 4 tu kwasababu Mgambo wana 28.

Kutokana na Azam kuteleza mechi tatu wakivuna pointi tatu tu, wamekaribiana sana na Simba, kitu kilichompa nguvu kocha mkuu wa Wanamsimbazi, Goran Kopunovic nguvu ya kuisaka nafasi ya pili.

Kwa miaka miwili Simba hawajapanda ndege kwenda kucheza mechi za kimataifa. Kumbuka kwa mara ya mwisho kutwaa ubingwa ni msiamu wa 2011/2012. Msimu uliofuata (2012/2013) walishika nafasi ya tatu Azam wakishika nafasi ya pili, Yanga wakitwaa ubingwa.

Msimu wa 2013/2013 Simba walishika nafasi ya nne, ya tatu ikashikwa na Mbeya City, ya pili Yanga na bingwa akawa Azam fc.

Bila shaka wanataka kufuta makosa baada ya Azam kuwapa mwanya.

Kwa kuanza harakati zao wanachuana na Mbeya City uwanja wa Sokoine keshokutwa katika mechi ya ligi kuu.

Kocha Kopunovic amesema: “Sasa kuna mwanga mbele yetu, kama tutashinda mechi 5 zilizosalia kuanzia ya Mbeya City tunaweza kukaa nafasi nzuri kutegemeana na matokeo ya Azam. Imekuwa safari ndefu, lakini tumekuwa tukiimarika kadri siku zinavyokwenda”.

“Mbeya City ni timu nzuri, wametoka kufungwa na Yanga ingawa walicheza soka zuri, tumekuwa na muda kidogo wa kujiandaa toka tulipocheza na Kagera, tuko tayari kwa ajili ya mechi, tuwaambia mashabiki wangu, mashabiki wa Simba, tuwape moyo vijana wetu”.

Kwa upande wa kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema: “Tunamshukuru Mungu tunaendelea vizuri na maandalizi yetu kuisubiri Simba jumamosi, utakuwa mchezo mgumu, lakini siku zote sisi tunajiandaa kwa mechi 26 za ligi. Tumeacha pointi tatu Dar es salaam, lakini kumbuka tulichukua 3 kutoka kwa Simba, tunajitahidi kutumia vizuri faidi ya nyumbani na tunaamini tutashinda”.

Kama Mbeya City watashinda itakuwa jambo zuri kwako katika harakati za kukwepa kushuka daraja, lakini Simba wakishinda watazidi kuwachanganya Azam katika nafasi ya pili.


Azam wao watacheza dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa Azam Complex.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video