Baada ya hapo jana kutangaza kuwa ataachana na klabu ya Borussia
Dortmund mwishoni mwa msimu huu,kocha Jurgen Klopp amefunguka
tena na kusema hatachukua muda wa mapumziko kama wengine wanavyodhania.
Kocha huyo alitua klabuni hapo mwaka 2008,ameiwezesha klabu hiyo
kuchukua ubingwa wa Bundesliga mara 2,mwaka 2011 na 2012 na ubingwa wa
DFB Pokal na pia kuiwezesha timu hiyo kushika nafasi ya pili katika
michuano ya klabu bingwa Ulaya msimu wa 2012/2013.
Klopp,47, amesisitiza kuwa hatafanya kama Pep Guardiola ambaye
alipumzika kwa mwaka mmoja baada ya kutoka katika klabu ya Barcelona
mwaka 2012.
Taarifa hiyo imewastua watu wengi na kuwafanya wadau wa soka kudhani
kuwa kocha huyo atachukua mikoba ya Manuel Pellegrin ambaye anasuasua
katika klabu ya Manchester City. "Siyo kwamba nimechoka, pia sijafanya
mazungumzo na klabu yoyote mpaka sasa. Sihitaji kuchukua mwaka mmoja wa
mapumziko" alisema Klopp.
Baada ya kutolewa katika michuano ya klabu bingwa msimu huu,klabu ya
Borussia Dortmund inayoshika nafasi ya 10 katika msimamo wa ligi kuu
nchini Ujerumani sasa inajitahidi kufanya vizuri ili waweze kumaliza
wakiwa katika nafasi za juu kunako ligi hiyo.

.jpg)
0 comments:
Post a Comment