Monday, April 13, 2015


NADIR HAROUB ALI ‘Cannavaro’ , nahodha wa Young Africans alifunga goli moja katika ushindi wa 3-1 waliopata Yanga dhidi ya Mbeya City jana uwanja wa Taifa.

Magoli mengine yalifungwa na Kpah Sherman na Salum Telela wakati la Mbeya City lilifungwa na Themi Felix.

Cannavaro ‘Baba mwenye nyumba’ safu ya ulinzi ama kamanda wa ngome ya ulinzi ya Yanga baada ya mechi hiyo ametamka kauli mbili kubwa;

Moja ni kuhusu upinzani walioonesha Mbeya City fc ambapo amesema:

“Mimi nasema kwamba watu wa mbele waongeze umakini, ila tu Mbeya City ni timu nzuri, wamecheza vizuri sana, ila sisi ni wazuri zaidi yao, nafasi imepatikana na tumetumia”.

Kauli ya pili ni kuhusu mechi ya kombe la Shirikisho dhidi ya Etoile du Sahel itayopigwa wikiendi ya wiki hii, Cannavaro amesema: “Bado tuna mchezo mgumu wa kimataifa (kombe la Shirikisho dhidi ya Etoile du Sahel ya Tunia) na tunajiandaa kwa ajili ya mchezo huo”

Cannavaro ni miongoni mwa mabeki wa kutumainiwa wa Yanga na amekuwa kiongozi mzuri wa kuhamasisha timu kila inapocheza, iwe mechi za ligi kuu au za kimataifa.


Pia ni mchezaji muhimu timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video