Wednesday, April 29, 2015


AZAM FC imetamba kuzing’ang’ania pointi 9 zilizosalia katika michezo yao mitatu iliyobakia kuhitimisha msimu huu wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Kocha msaidizi wa Azam, Dennis Kitambi amesema kufanya vibaya kwao kumechangiwa na ratiba ngumu ya ligi kuu.
“Ulishawahi kuona wapi timu inacheza mechi nne za mashindano ndani ya siku 11? Hakika ulikuwa mzigo kwetu kwasababu tulikuwa tunalazimika kusafiri, mara Morogoro mara Tanga, tunarudi tena Dar. Ratiba haikututendea haki”. Amesema Kitambi na kukiri; “Tumeshapoteza ubingwa wetu, lakini sasa tunataka nafasi ya pili. Tuna hamu ya kukutana na Simba na Yanga, tunataka kuchukua pointi zote ili kuchukua nafasi ya pili kwa kishindo”.
Mwishoni mwa juma hili Azam wenye pointi 45 baada ya kucheza mechi 23 watachuana na Simba uwanja wa Taifa na mei 6 mwaka huu watakabiliana na Yanga kabla ya kumaliza msimu kwa kuchuana na Mgambo JKT mei 9 mwaka huu.
Simba wanashika nafasi ya tatu kwa pointi 41 baada ya kucheza mechi 24 na wamebakiwa na mechi hiyo dhidi ya Azam na JKT Ruvu, mechi zote zitapigwa uwanja wa Taifa

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video