Monday, February 16, 2015

MAAFANDE wa Tanzania Prisons wametamba kutowahofia Yanga katika mechi yao ya ligi kuu Tanzania bara itayopigwa uwanja wa CCM Sokoine, Mbeya alhamisi februari 19 mwaka huu.

Kocha mkuu wa Prisons, David Mwamwaja amesema waliweka kambi Dar es salaam wakijua watacheza na Azam fc jumapili ya wiki hii, lakini wamepata taarifa mapema leo kuwa watakuwa na mchezo dhidi ya Yanga, uwanja wa Sokoine Alhamisi ya wiki hii, hivyo wamelazimika kusafiri haraka kurudi Mbeya.

“Timu ilikuwa Dar es salaam, imesafiri leo na imeingia jioni hii Mbeya. Tunajipanga kwa ajili ya Yanga. Tulifika huko Dar es salaam kwaajili ya mchezo dhidi ya Azam, lakini tulipoambiwa tunacheza na Yanga Sokoine Mbeya ikabidi tuje Mbeya leo”. Amesema Mwamwaja.


Kuhusu mechi yenyewe, Mwamwaja amesema: “Tunaifahamu Yanga, na wao wanatufahamu vizuri, hawawezi kutubeza. Tuko nyumbani lazima tupambane kupata ushindi, tumepata sare nyingi lakini ni bora kuliko kupoteza. Mimi bunduki zangu zipo sawa, nitatumia vijana wa chini ya miaka 20 nikiwachanganya  na kaka zao”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video