KAGERA Sugar imefurahia kushika nafasi ya tatu
katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kuichapa JKT Ruvu bao
1-0 jana uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga.
Matokeo hayo yameifanya Kagera Sugar ifikishe
pointi 21 katika nafasi ya tatu, pointi nne nyuma ya vinara Azam fc na Yanga
waliopo nafasi ya pili kwa pointi 25, lakini wanazidiwa mabao ya kufunga na
kufungwa.
Simba wameshika nafasi ya nne kwa kujikusanyia
pointi 20 na hii ni kutokana na ushindi wa mabao 2-0 waliopata jana uwanja wa
Jamhuri Mkoani Morogoro dhidi ya wenyeji Polisi Moro.
Kocha msaidizi wa Kagera Sugar, Murage Kabange
amesema sasa wanaelekeza nguvu katika mechi yao ya mwishoni mwa wiki dhidi ya
Polisi Moro uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga.
“Tunashukuru tumeshinda jana dhidi ya JKT Ruvu.
Bao la ushindi lilifungwa na Atupele Green dakika ya 30”. Amesema Kabange na
kuongeza. “Ushindi huu umetuweka nafasi ya tatu, ni jambo jema na tunatakiwa
kuongeza juhudi zaidi”.

0 comments:
Post a Comment