JUZI kwenye Uwanja wa Azam jijini hapa kulikuwa na mechi kali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika ikiwahusisha wenyeji Azam FC dhidi ya E-lMerrikh ya Sudan.
Azam FC waliibuka na ushindi wa mabao 2-0. Shukrani kwa mabao ya kinara wa mabao Ligi Kuu Tanzania Bara kwa sasa, Mrundi Didier Kavumbagu na mshambuliaji mtokea benchini, John Bocco 'Adebayor' yaliyopeleka msiba kwa mabingwa hao mara 19 wa Ligio Kuu ya Sudan.
Takwimu za mechi hiyo zinaonesha wageni waliongoza kwa kumiliki mpira na kucheza kwa nidhamu kubwa bila. Takwimu zote za mechi hiyo ziko hapo chini. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa Kituo cha Azam TV kilichorusha moja kwa moja 'live' mechi hiyo ya kimataifa.
Mashuti yayolenga goli
Azam 10-10 El-Merrikh
Mashuti yasiyolenga goli
Azam 4-5 El-Merrikh
Kona
Azam 3-9 El-Merrikh
Rafu/Faulo
Azam 16-10 El-Merrikh
Kuotea
Azam 6-1 El-Merrikh
Kadi za Njano
Azam 1-1 El-Merrikh
Kadi Nyekundu
Azam 0-0 El-Merrikh
Kumiliki mpira
Azam 48%-52% El-Merrikh

0 comments:
Post a Comment