
BAADA ya kupita miaka 27, Mwadui FC imerejea ligi kuu Tanzania bara baada ya
kuitandika Burkifaso mabao 4-1 katika mechi ya mwisho ya ligi daraja la kwanza
iliyopigwa leo uwanja wa Mwadui, Shinyanga.
Mwadui inarudi ligi kuu ikiwa chini ya kocha
Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’ ambaye ametamba kutwaa ubingwa msimu ujao.
Mbali na Mwadui, timu nyingine zilizopanda ligi
kuu msimu ujao ni Toto Africans ya Mwanza, Majimaji ya Songea na African Sports
ya Tanga.
Cha kufurahisha zaidi ni kwamba timu zote
zilizopanda mwaka huu zilikuwepo ligi kuu miaka ya nyuma.
Hakuna timu mpya kabisa iliyopanda kama ilivyokuwa
kwa misimu michache iliyopita ambapo timu kama Stand United, Mbeya City
zilipanda ligi kuu.
Ligi kuu msimu ujao itakuwa na jumla ya timu 16 na
timu mbili zitashuka daraja msimu huu.

0 comments:
Post a Comment