



Dakika ya 86 Makorongoni walipata goli la pili na likiwekwa wavuni na David Mhanga aliyekuwa mchezaji bora wa mechi hiyo baada ya kuwapiga chenga mabeki wa Kata ya Kitanzini na kumchanganya kipa wa Kitanzini Abel.

Magoli hayo yaliwavunja nguvu kata ya Makorongoni na dakika ya 90 alikuwa David Mhanga tena aliyewahakikishia Makorongoni ubingwa wa kwanza wa mashindano ya Kombe la Hepautwa kwa kufunga goli la tatu na ushindi katika fainali hiyo.
Kwa ushindi huo timu ya Makorongoni imefanikiwa kujinyakulia kitita cha shilingi 1,000,000 na kombe , mshindi wa pili timu ya Kata ya Kitanzini walijipatia shilingi 600,000 na mshindi wa tatu kata ya Kihesa aliondoka na shilingi 300,000.
Mdhamini wa mashindano hayo Nuru Hepautwa akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi alizishukuru kata zote kwa kushiriki na kuahidi mwakani kuyaboresha zaidi katika vipengele vya zawadi na kuwataka wachezaji kujituma zaidi kutumia michezo kama ajira itakayowakomboa katika umaskini.


0 comments:
Post a Comment