Sunday, September 7, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam



0712461976
YANGA SC chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo ilitarajia kucheza mechi ya mwisho ya kimataifa ya kirafiki  dhidi ya Big Bullets (zamani Bata Bullets)  ya Malawi leo uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kufikia jana usiku, uongozi wa Yanga kupitia kwa Afisa habari wake, Baraka Kizuguto ulikaririwa na vyombo vya habari kuwa maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo yamekamilika kwa mujibu wa waandaaji DRFA.

Kwa tafsiri ya haraka haraka tayari Yanga walikuwa wanawasiliana na chama cha soka cha mkoa wa Dar es salaam, DRFA, kuhusu ujio wa Big Bullets na ndio maana Kizuguto alisema kila kitu kinakwenda sawa na kuwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi leo.

Mpaka kufikia mapema leo asubuhi, mashabiki walitambua uwepo wa mechi hiyo, lakini ghafla taarifa kutoka Yanga zinaeleza kuwa mchezo huo haupo tena kwasababu Wamalawi hawajawasili nchini.

Taarifa ya Yanga katika ukurasa rasmi wa mtandao wa kijamii imesomeka:

“KUMRADHI: Wapenzi, wanachama, washabiki na wadau wa soka kwa ujumla, mechi kati ya Young Africans dhidi ya Big Bullets iliyokua ifanyike leo haitakuwepo.

Kwa mujibu wa waandaji wa mchezo huo DRFA timu ya Big Bullets imeshindwa kuwasili nchini, na jitihada za kupata timu nyingine imeshindikana.


Tunawaomba radhi kwa usumbufu wote ambao umejitokeza.

Daima Mbele Nyuma Mwiko”.

Kutokana na suala hilo, binafsi kuna baadhi ya mambo nimeona ni vyema kuyasema ili yasijirudie tena;

Mosi; ucheleweshaji wa taarifa kwa mambo muhimu kama mechi ya leo ni kuwakosea haki wapenzi na wadau wa soka.

Kwanini mpaka kufikia jana usiku DRFA wasijue kama Big Bullets hawaji nchini?, labda kama waliwaambia watakuja siku hiyo hiyo ya mechi.

Lakini hata kama ni hivyo, kwanini hawakuthibitisha kama usafiri wa uhakika upo kwa Big Bullets kufikia jana?

Zikiwa zimesalia takribani saa tano kuanza kwa mechi, taarifa kama hii inatoka, kweli ni uungwana?

Sikatai, yawezekana ni sababu zilizo nje ya uwezo wa kibinadamu, lakini kwa watu wenye kujua majukumu yao vizuri walitakiwa kujua mpaka kufikia jana.

Najaribu kujenga hoja ya kuleta usumbufu mkubwa, Fikiria muda huu mtu anatoka mikao ya jirani, Tanga, Morogoro, Pwani kuja kuangalia mechi, halafu kwa bahati mbaya hana chanzo cha habari, anatua Ubungo wanamwambia mechi haipo. Ni haki kwake?

Kwa hili DRF wamechemsha, wala hakuna haja ya kupepesa macho. Siku nyingine wajipange.

Mechi kubwa kama hii inatakiwa timu pinzani iwepo siku moja au mbili kabla. Mambo ya siku ya mechi ni usanii tu.

Kama watu walishakata tiketi kabisa itakuwaje? Watarudishiwa kwasababu hakuna uhakika wa mechi nyingine? Au ndio moja kwa moja?

Hakika kuna mambo yanayotakiwa kupigwa vita kama ubabaishaji huu.

DRA kama waandaaji, lawama zote mnabeba ninyi na kwa sehemu Fulani Yanga.

Pili; Viongozi wa Yanga wanatakiwa kuwa makini kufuatilia taarifa muhimu kuhusu klabu yao.

Yawezekana DRFA wamewaangusha kwasababu wao ndio walikuwa na dhamana ya mechi hiyo, lakini kama wahusika wakuu walitakiwa kufuatilia kwa ukaribu zaidi kwa manufaa ya mashabiki wao.

Inawezekana DRFA wakachukiwa na wapenzi wa Yanga, lakini hata viongozi wao wanatakiwa kubeba sehemu ya lawama hizo.

Kwanini mpaka kufikia jana walikuwa hawana uhakika na wakawatangazia mashabiki wao kuwa mechi ipo? Hapa walitakiwa kuwa watulivu na kuulizia mara kwa mara ili kutoa taarifa rasmi jana.

Kwa bahati mbaya sana kuna baadhi ya viongozi walikaririwa wakisema Big Bullets imewasili nchini, lakini kumbe hawajui kitu.

Sawa na tamasha la ‘Coastal Day’ leo hii septemba 7, makamu mwenyekiti wa Coastal alikaririwa jana akisema hajui chochote kuhusu siku hiyo.

Kama kiongozi wa juu hajui siku kama hiyo, unadhani kuna uongozi hapo? Taarifa jambo jema sana jamani.

Ni kweli Yanga na DRFA walikuwa na mawasiliano ya mara kwa mara mpaka kufikia jana?

Sijui, lakini kwa haya yaliyojitokeza, kuna shaka juu ya hilo

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video