Anafiti wapi? Radamel Falcao akipozi katikia picha na Ryan Giggs baada ya kusajiliwa siku ya mwisho ya usajili.
GWIJI wa Manchester United, Paul Scholes haoni namna ambavyo kocha Louis van Gaal ataweza kuwatumia Wayne Rooney, Robin van Persie na Radamel Falcao katika timu moja.
Scholes anaamini kwamba Falcao, ambaye alisajiliwa dakika za mwisho za dirisha la usajili wa kiangaizi mwaka huu, ni mchezaji wa kipekee, lakini amesisitiza kuwa timu yake hiyo ya zamani itakuwa na uwezo wa kuwachezesha washambulaiji wawili tu wenye majina makubwa na si watatu.
Katika kolamu yake anayoandika katika gazeti la The Independent, Scholes alisema: "Nilipomtazama Falcao wakati anaichezea Porto, Atletico Madrid na Monaco, niliona mshambuliaji mwenye ubora wa juu na mwenye rekodi nzuri ya ufungaji wa mabao ambayo ipo katika dunia hii"
Nani atakaa benchi? Paul Scholes haamini kama Louis van Gaal ataweza kuwaanzisha kwa pamoja nyota wake watatu.
"Falcao ameleta ushindani katika safu ya ushambuliaji ya United. Hakuna jinsi ya Van Gaal kuwatumia kwa pamoja
Rooney, Van Persie na Falcao. Italazimika kuwatumia wawili kati ya watatu na wawili hao ni ngumu kusema ni nani".

0 comments:
Post a Comment