Sunday, September 7, 2014

BAO pekee la Musa Hassan Mgosi limeipa Mtibwa Sugar ushindi wa 1-0 dhidi ya Ndanda fc katika mchezo wa kirafiki uliopigwa jioni ya leo uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Msemaji wa Mtibwa Sugar, Tobias Kifaru Ligalambwike amesema Mgosi alifunga bao hilo kipindi cha pili kwa shuti kali.

Licha ya kufungwa, Kifaru alisema Ndanda walijitahidi kucheza soka safi, lakini walizidiwa maarifa na mabingwa hao wa mwaka 1999 na 2000.

Kifaru aliongeza kuwa  Mtibwa ni timu kubwa na ndio maana Simba waliikimbia na kucheza na timu dhaifu ya Gor Mahia ambayo waliishinda mabao 3-0 jana uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video