Friday, September 5, 2014

Kocha mkuu wa Yanga sc, Marcio Maximo (kushoto) akimuelekeza jambo mshambuliaji wa klabu hiyo, Jeryson John Tegete

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


0712461976

KATIKATI ya wiki hii, Yanga sc ilishuka dimbani kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Thika United kutoka nchini Kenya katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na kushinda bao 1-0.

Bao pekee la Mbrazil, Geilson Santos Santana ‘Jaja’ katika dakika ya 60 lilitosha kumpa kocha wa Yanga, Marcio Maximo ushindi wa nne mfululizo katika mechi nne za kirafiki ilizocheza mpaka sasa.

Katika mchezo huo kuna mapungufu kadhaa yalijitokeza katika kikosi cha Yanga hususani kipindi cha kwanza, lakini nadhani ilichangiwa na ubora wa Thika United ambayo ilionekana kucheza kitimu zaidi kwasababu ipo katika ligi inayoendelea wakati wanajangwani wanatengeneza timu.

Kuna mambo matatu Maximo huwa anapenda kusema kila baada ya mchezo.

Moja ni kutokuwa tayari kumzungumzia mchezaji mmoja mmoja katika kikosi chake.

Pili ni kuepuka kuzungumza mapungufu ya timu hadharani, akiamini njia nzuri ni kuzungumza nao katika kikao cha ndani baada ya mechi.

Tatu ni kutokuwa na wachezaji wenye namba za uhakika badala yake kuwa na kundi la wachezaji wenye utayari wa kutumika muda wowote.

Ninavyomfahamu Maximo ni kocha anayependa kuongoza timu yenye morali kubwa na hapendi kuona kuna mpasuko miongoni mwa wachezaji.

Zipo sababu nyingi zinazochangia timu kuwa na morali, mojawapo ni kuzungumza na wachezaji kama timu na sio kushusha lawama kwa baadhi ya wanandinga wanaofanya vizuri.

Marcio Maximo (katikati) akiwa na wachezaji wake kisiwani Pemba walipoweka kambi ya siku tano na tano nyingine kisiwani Unguja

Kuna baadhi ya makocha wa ndani na kimataifa huwa wanazungumza na mchezaji mmoja mmoja pale yanapotokea makosa binafsi na anamuagiza cha kufanya bila wenzake kujua.

Hii inatokea pale ambapo kocha anagundua kuna sababu binafsi zilimfanya mchezaji wake acheze chini ya kiwango au kufanya makosa binafsi uwanjani.

Maximo kwa upande wake anasema hataki kumzungumzia mchezaji mmoja mmoja kwasababu timu inaundwa na wachezaji 11 uwanjani.

Makosa ni sehemu ya mpira na ili ufunge goli lazima mpinzani akosee na ili ufungwe goli lazima wachezaji wa timu yako wakosee.

Mapungufu uwanjani ni jambo la kawaida na linatokea duniani kote, lakini baadhi ya makocha wanashindwa kutatua matatizo hayo kwa busara badala yake wanawabebesha lawama baadhi ya wachezaji.

Jambo hilo huwafanya wachezaji waingiwe na uoga na kujikuta wakishindwa kucheza mpira vile wanavyofikiria wakihofia lawama kutoka kwa kocha.

Ili kuepusha hilo, Maximo anapenda kuzungumzia ‘kufeli’ kwa timu kama timu na sio makosa binafsi ya Nadir Haroub au Kelvin Yondani.

Kosa la Mrisho Ngasa linajadiliwa kama timu na sio kumzungumzia Ngasa kwa makosa yake binafsi.

Marcio Maximo anasema hakuna mchezaji mwenye namba ya uhakika

Hili ni jambo zuri na litazidi kuipa nguvu Yanga kama timu na wachezaji watakuwa huru kucheza mpira kwa maelekezo ya Maximo.

Jambo la pili ni Maximo kutumia vikao vya ndani kuzungumza mapungufu ya wachezaji na kuwaagiza nini cha kufanya mechi zilizopo mbeleni.

Ni jambo la busara zaidi kuliko kuanika kila kitu hadharani. Kuna baadhi ya makocha wanashindwa kuvumilia na kujibu kila wanaloulizwa.

Ni kawaida kumsikia kocha akizungumzia mapungufu ya timu, lakini waliowengi wanatumia zaidi nafasi husika na sio kutaja moja kwa moja mchezaji aliyechemsha.

Kocha anaweza kusema timu yangu ilikuwa na matatizo safu ya ulinzi au kiungo, lakini ni mara chache kumzungumzia mchezaji mmoja mmoja tu.

Kila mtu ana mtazamo wake kuhusu soka na kwa bahati mbaya waliowengi tunajifanya tunajua zaidi ya makocha, lakini ukweli unabakia palepale kuwa mashabiki wengi wa soka huwa hawana utaalamu wa kiufundi na kimbinu katika soka.
Ni rahisi kumsikia shabiki akishusha lawama kwa mchezaji mmoja anapofanya makosa na kupiga kelele atolewe, lakini ni ngumu kujua kwanini kocha anaendelea kumtumia uwanjani licha ya wengi kuona hafai.

Mwalimu anapanga wachezaji kutokana na aina ya mpinzani wake, na ndio maana unaweza kuona mchezaji fulani hachezi mara kwa mara, lakini kuna mechi anapangwa kwa dakika zote 90.

Kocha anaelewa kuwa atasaidia kupata matokeo kuliko mnayemtaka ninyi, lakini linapotekea kosa, mwalimu ana namna ya kuzungumza na mchezaji huyo.

Ndio maana Maximo anatambua kuwa mapungufu ya wachezaji lazima waambiwe wao. Kuna maana gani kuzungumzia kila kitu kwenye vyombo vya habari.

Kuna faida gani umma wa wapenda michezo kujua kila kitu kuhusu mapungufu ya timu? Kwani wao wana nafasi gani?

Kazi ya shabiki ni kushangilia mpira tu unaochezwa na wachezaji kwa kuzingatia falsafa ya mwalimu wao.

Mambo ya kimbinu na kiufundi ni kocha na wachezaji wake, hivyo hakuna haja sana kumwambia shabiki mapungufu ya wachezaji badala ya kuwaambia wao wenyewe.

Ni jambo nzuri kukosolewa katika kikao cha ndani kuliko kukosolewa hadharani. Kuna watu hawana uvumilivu, ukikosolewa hadharani nao huongezea kwa kuponda zaidi.

Kupondwa pia huwapunguzia ufanisi wachezaji, hivyo njia bora ni kukaa nao kwa busara bila watu kujua nini mmezungumza.

Kwa hili Marcio Maximo nadhani yuko sahihi na itamsaidia sana kujenga morali ya wachezaji wake.

Kitu kingine muhimu alichofanya Maximo ni kuwafanya wachezaji wote wajitume kwasababu hakuna mwenye uhakika wa namba.

Maximo anapenda kuwa na kundi la wachezaji wenye uwezo wa kutumika muda wowote, hivyo anawajenga wachezaji wote katika utayari wa kucheza.

Moja ya matatizo ya timu za kibongo ni kuwa na idadi ya wachezaji Fulani wenye uhakika wa namba, lakini wengine wanakamilisha idadi tu ya wachezaji wa timu.

Mchezaji anakaa msimu mzuri bila kucheza mechi yoyote, siku akiingia uwanjani kutokana na kukosekana kwa mchezaji muhimu, unamuona kabisa akitetemeka.

Madhara ya kuwa na wachezaji wenye namba za uhakika na wengi kutokuwa na uhakika wa kucheza ni pale inapotokea majeruhi, kocha anashindwa cha kufanya kwasababu waliopo benchi hawajiamini.

Maximo kuwaaminisha wachezaji wote kuwa wana nafasi ya kucheza, ni jambo muhimu na litafanya wote wajiamini na kujituma zaidi.

Lakini ukweli ni kwamba kuna nafasi huwa zina watu wake na si rahisi kumchomoa mchezaji.

Timu lazima iwe na wachezaji wa kikosi cha kwanza, ndivyo ilivyo duniani kote, lakini ni jambo zuri kuwa na timu yenye kundi kubwa la wachezaji wenye utayari wa kucheza.

Kwa hili pia, Maximo anaendelea hisia nzuri kwa wachezaji wa Yanga na itamsaidia kufanikiwa malengo yake.

Wakati huo huo,timu ya Young Africans itashuka dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam siku ya jumapili kucheza mchezo wake wa mwisho wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya Big Bullets FC (zamani Bata Bullets) inayoshiriki Ligi Kuu ya TNM nchini Malawi.

Siku ya jumapili mechi inatarijiwa kuanza majira ya saa 10 kwa saa za Afrika Mashariki na viingilio vya mchezo ni kama ifuatavyo:

VIP A Tshs 30,000/=

VIP B & C Tshs 20,000/=

Orange Tshs 10,000/=

Blue & Green Tshs 5,000/= 



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video