Wednesday, September 10, 2014

NASSIB Abdul ‘Diamond Platnumz’ ni msanii wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Fleiva’ anayetikisa ndani na nje ya nchi kwa sasa.

Mkali huyu wa kibao cha ‘Number One na Mdogo mdogo’ amejizolea umaarufu mkubwa na kuteka soka la mashabiki nchini Tanzania, nchi za Afrika mashariki na kati, sehemu kadhaa za Afrika magharibi na kwingineko, bila kusahau duniani kote.

Kutokana na ufanisi wa kazi zake, Diamond amekuwa msanii wa kipekee na anakusanya mkwanja mrefu pengine kuliko wasanii wote, kwa rekodi za miaka ya karibuni.

Lakini wengi wakisikia jina la Diamond, basi wanarejea vibayo vyake vingine vya sasa na zamani. Nyimbo kama Nenda kamwambie, Mbagala, Nalia na Mengi, Mawazo, Nimpende Nani, Ukimwona, Nataka kulewa, My Number One na sasa Mdogo Mdogo, hakika zinapigwa na kusikilizwa sana.

Pia amekuwa na shoo za bei mbaya ndani na nje ya nchi. Hutumika katika matangazo ya makampuni makubwa na kuingiza pesa ndefu.

Yapo mengi ya kumzungumzia Diamond katika maisha yake ya muziki, lakini leo tunaangazia maisha ya upande wa pili, hususani michezo.

Daimond anamkubali sana bondi Floyd Mayweather

Nyota huyu wa muziki alikiri kuwa zamani alikuwa anapenda sana michezo hususani mchezo wa ngumi,  lakini akaachana nao na kuingia katika soka.

Alisema: “Zamani nilikuwa napenda sana michezo,nilikuwa napenda ngumi ‘Boxing’,  lakini nikaona mambo ya kupigana hapana!”

“Pia nikaanza kucheza mpira. Nilicheza vizuri tu, lakini kuna vitu vilinikatiza hasa mama yangu ambaye hakupenda nicheze mpira. kwasababu kuna jirani yetu alipata matatizo, waligongana miguu na akavunjika.”

“Kila nikitaka kuendelea kucheza, basi mama anasema unafahmu fulani alivunjika kwasababu ya mpira, kila nikifiria daaah! Nilikuwa naogopa na kuona kweli naweza kuvunjika miguu. Kuanzia hapo nikaacha kabisa mpira mpaka leo na nikawa napenda muziki”

Kama ilivyo kawaida kwa vijana wengi, huwa wanapenda kuzishabikia klabu kongwe mbili nchini, Simba na Yanga, kwa upande wa Diamond hali ikoje?

“Nilipokuwa mdogo nilikuwa nafuatilia Simba, lakini ilikuwa mkumbo. 
Mrisho Ngassa

Nikisikia wengine wako Yanga basi namimi Simba, lakini nilikuwa sielewi.”

“Kiukweli sijui ni timu ipi kwasababu sijakaa sana kafuatilia. Nisikia watu wengi wapo Yanga, kwahiyo naona nikisema Yanga nitakuwa kama nimefuata mkumbo”. Alisema Diamond.

Kichekesho cha aina yake ni kwamba, katika wachezaji wote wanaocheza soka la Tanzania kwa sasa, Diamond anamjua mchezaji mmoja tu  ambaye ni mshambuliaji wa Yanga na Taifa Stars, Mrisho Khalfan Ngassa.

“Ngassa mwanangu. Nilikuwa nasikia anatajwa sana, nikaja kukutana naye na tukafanya Tangazo. Nikaona ni mtu poa na kuanzia hapo akawa mwanangu. Muda mwingi akawa ananipigia akisema mwanangu sisi tunaenda kucheza mpira sehemu fulani”

“Kwahiyo ukisema niangalie mpira, nitasema Ngassa tu kwasababu ndio ninayemfahamu na ni mwanangu”.

Kama kawaida, wasanii wengi kama akina Madee, Chege, Professor Jay na wengine wanafuatilia sana klabu za nje kama Manchester United, Liverpool na nyinginezo, lakini kwa Diamond je?

“Kuna kipindi nilikuwa nakaa Kariakoo na nilikuwa naipenda sana Barcelona kwasababu alikuwepo huko Eto’o. Mpaka sahizi najua Messi yupo, na siku za karibuni, Neymar. Zamani nilikuwa naweza kutaja namba zote, lakini sahizi sikumbuki” alisema mwanamuziki huyo maarufu.

Kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, Diamond amewafuata baadhi ya wachezaji nyota kama Samuel Eto’o, Didier Drogba, Emmanuel Adebayor, na bondi Mayweather, kwanini hao na sio watu wengine?

“Nimekuwa nikiwasikia sana. Wanacheza halafu ni ‘mastaa’. Kila nikipita mitaani nawasikia, basi nikaona ngoja niwafuate” Alisema Diamond.

“Kuhusu Myweather, yaani ni mtu staa sana, mtu wa mashauzi kinoma, matanuzi, ananifurahisha sana. Mara aposti mademu zake, mara magari yake, fedha zake…nampenda sana”.

Wapenzi wengi wa soka ukiwapa nafasi ya kuchagua ni mchezaji gani wana ndoto ya kuonana naye ana kwa ana, kila mtu atataja wake kutokana na mapenzi makubwa aliyonayo, kuhusu Diamond hali ikoje?


“Nina ndoto ya kukutana na Messi kwasababu namjua toka anaanza Barcelona, alivyoanza kuchez mpaka anakuwa staa. Ni mtu wa kazi. Kwa juzi juzi alipokosa tuzo ya mchezaji bora wa dunia, iliniuma sana”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video