Saturday, August 16, 2014

Kikosi cha JKT Ruvu Stars msimu uliopita

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Agosti 16, 2014, saa 6:49 mchana

MAAFANDE wa JKT Ruvu Stars kutoka mkoani Pwani wanashuka dimbani jioni ya leo kukipiga dhidi ya wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika mechi ya kirafiki itakayocheza uwanja wa Bandari Tandika jijini Dar es salaam majira ya saa 10:00 jioni.

Waandaaji wa mechi hiyo wamesema kiingilio katika mtanange huo unaozikutanisha timu mbili za ligi kuu Tanzania bara ni buku tu (1,000/=)

Kocha wa JKT Ruvu, Fredy Felix Minziro amesema maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo yanakwenda vizuri na wanatarajia kupata kipimo kizuri kutoka kwa Mtibwa Sugar.

“Maandilizi yamekwenda vizuri kwa maana ya kwamba,  tumepata kikosi kizuri. Juzi tulicheza mechi ya kirafiki na Polisi Morgoro na kushinda mabao 3-1”. Alisema Minziro.

“Kupata timu ya ligi kuu ni nafasi nzuri ya kuwaona vijana wangu, nadhani mechi dhidi ya Mtibwa Sugar itakuwa kipimo kizuri na tutapata mazoezi mazuri’

Kuelekea msimu ujao wa ligi kuu, Minziro alisema kikosi chake kitafanya vizuri kutokana na maandalizi ya muda mrefu wanayoendelea nayo mpaka sasa.

“Ninaamini wachezaji watafanya vizuri msimu ujao kwasababu wanaonesha kuimarika. Nina mpango wa kucheza mechi za kirafiki dhidi Ruvu Shooting, Simba na Yanga kama watakuwa tayari”.

Kwa upande wake kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime alisema mechi ya leo ni kipimo kizuri kwake kwasababu JKT Ruvu ni timu bora.

“Sisi tunaendelea vizuri na maandalizi na tunacheza na JKT Ruvu.Tunaamini itakuwa mechi nzuri”. Alisema Mexime.


“Ruvu tunawaheshimu, lakini tumesajili vizuri na tutaonesha burudani nzuri. Niwaombe mashabiki wafike kwa wingi kuona mpira wa kiwango cha juu” 

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video