Sunday, August 3, 2014


Imechapishwa Agosti 3, 2014, 2014, saa 11:27 jioni

KLABU ya Simba imefanya mkutano mkuu wa wanachama leo hii katika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Osterbay jijini Dar es salaam kujadili masuala mbalimbali ya klabu hiyo.

Mkutano huo ni wa kwanza tangu viongozi wapya chini ya Rais Evans Eliaza Aveva na makamu wake Geofrey Nyange ‘Kaburu’ waingie madarakani juni 29 mwaka huu.

Agenda za mkutano huo zilitangazwa jana na Agenda ya 11 ambayo ilihusu wanachama 72 waliosimamishwa uanachama na kamati tendaji ilitegemewa kuwa ya vuta ni kuvute.

Kama ilivyotabiriwa jana, leo hii agenda hiyo ilivuta hisia za wengi na mwisho wa siku taarifa kutoka kwenye mkutano huo zinaeleza kuwa mkutano mkuu umeamua kuwafuta uanachamama (kuwafukuzwa) wale wote walioipeleka Simba mahakamani.

Idadi ya wanachama 72 pamoja na aliyekuwa mgombea wa Urais wa klabu hiyo, Michael Richard Wambura wamefutwa na kufukuzwa kabisa.

Taarifa zinaarifu kuwa maamuzi hayo yamechukuliwa na wanachama zaidi ya 600 waliohudhuria mkutano huo.

Wambura aliipeleka Simba mahakamani mwaka 2010 wakati wanachama wengine waliobaki waliipekea klabu mahakama kuu kanda ya Dar es salaam  wakitaka uchaguzi mkuu uliofanyika juni 29 mwaka huu usimamishwe kwa madai kuwa katiba ilikiukwa na kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya mwenyekiti wake, mwanasheria, Dkt. Damas Wambura, lakini chanzo kikubwa kilikuwa kuenguliwa kwa Wambura.


Hata hivyo kabla ya ya kufikia maamuzi ya leo, Rais wa Simba Evans Aveva aliwataka wanachama waliosimamishwa kujitokeza kwake na kuwasilisha utetezi, lakini hakuna mwanachama aliyefanya hivyo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video