Monday, August 4, 2014

Imechapishwa Agosti 4, 2014, saa 12:10 jioni

MASHABIKI wa Zamalek walivamia makao makuu ya klabu hiyo na kuharibu mali za ofisi ya mwenyekiti, Mortada Mansour.

Mansour katika mkutano wake na waandishi wa habari aliwakosoa na kuwashutumu mashabiki wa klabu hiyo wanaojulikana kwa jina la ‘White Knights’.

“Kundi kubwa la mashabiki wa ‘White Knights’ lilivamia makao makuu ya klabu siku ya jumamosi mchana na waliharibu mali za ofisi ya mwenyekiti, lakini yeye hakuwepo.

“Waliharibu viti, milango na kuwaacha wafanyakazi wakiwa na hofu kubwa. Mfanyakazi mmoja wa klabu alijeruhiwa,” Mkurugenzi wa Zamalek, Alaa Mekled aliiambia Supersport.com.

“Tulizungumza na polisi na wataanza uchunguzi. Pia waliandika maneno mabaya kwenye ukuta yanayomtukana mwenyekiti” aliongeza.

Mwenyekiti wa klabu Mortada Mansour alisema: “Niliwaonya wasirudie tena kufanya hivyo, walinzi watawashughulikia. Hawa watoto sio mashabiki wa kweli wa klabu. Mashabiki wa kweli wanaiunga mkono klabu kwenye mechi zote ili kutafuta ushindi.


“Nilizungumza na waziri wa mambo ya ndani, Mohamed Ibrahim na nilimuomba walinzi wawe na bunduki kuilinda klabu. Kila siku kuna watu zaidi ya 500 wanakuja klabuni na lazima niwalinde.”

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video