Monday, August 4, 2014

MacDonald Mariga (kushoto) ameshindwa kuisadia Kenya kufuzu hatua ya makundi.

Imechapishwa Agosti 4, 2014, saa 12:37 asubuhi

WAKATI Tanzania ikitupwa nje ya michuano ya kufuzu fainali za mataifa ya Afrika, AFCON mwakani nchini Morocco na Msumbiji, Kenya nao walikalia kuti la moto baada ya kufurushwa na Lesotho.

Lesetho walifanikiwa kusonga mbele katika harakati za kusaka tiketi ya kucheza AFCON 2015 baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana na wenyeji Harambee Stars katika uwanja wa Taifa wa Nyayo mjini Nairobi jana jioni.

Mechi ya kwanza Lesotho walishinda bao 1-0 uwanja wao wa nyumbani, hivyo wamewatoa Kenya kwa wastani wa bao 1-0.

Sasa nchi hiyo inaungana na nchi za Gabon, Angola na wana fainali wa mwaka 2013, Burkina Faso katika kundi C, ambapo timu mbili za kwanza zitafuzu moja kwa moja kwenda Morocco mwakani.

Robert Sentongo alikuwa shujaa wa Uganda Jana

Nafasi ya Kenya ilikuwa finyu kwasababu walikosa motisha kutoka benchi la ufundi kwasababu kocha mkuu Adel Amrouche amefungiwa.

Kocha huyo raia wa Uholanzi anatumikia kifungo cha mwaka mmoja kwa kitendo chake cha kumtemea mate mwamuzi wa mechi katika mechi za mapema za kufuzu.

Kocha msaidizi, James Nandwa ndiye alikiongoza kikosi cha Harambee Stars .

Kama Lesotho watafanikiwa kufuzu fainali za AFCON 2015, itakuwa mara yao ya kwanza ksuhiriki michuano mikubwa ya Afrika katika historia yake.

Kwa upande wa Uganda, mambo yamewanyokea baada ya kufanikiwa kufuzu hatua ya makundi.


Uganda The Cranes walishinda mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza mjini Kampala dhidi ya Mauritania.

Katika mechi ya pili iliyopigwa jana jioni, Uganda ilishindi bao 1-0 ugenini, hivyo kusonga mbele kwa wastani wa mabao 3-0.


Bao pekee la Uganda lilifungwa na Robert Sentongo katika dakika tatu za nyongeza.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video