Nyota watatu: Luis Suarez akifanya mazoezi na Lionel Messi na Neymar kuelekea mechi ya kirafiki dhidi ya Leon.
LUIS Suarez amekutana na Lionel Messi na Neymar katika mazoezi ya Barcelona kujiandaa na mechi ya kirafiki kesho jumatatu.
Mshambuliaji huyo wa Uruguay kwasasa anaweza kufanya mazoezi na wachezaji wenzake baada ya mahakama ya juu ya rufani ya michezo CAS kusema kuwa FIFA haina mamlaka ya kumsimamisha kuhusu hilo.
Barcelona watakabiliana na timu ya Mexico ya Leon kesho katika mchezo wao wa mwisho wa maandalizi ya msimu.
Wikiendi ijayo wataanza kampeni za kusaka ubingwa wa La Liga dhidi ya Elche.
Mazoezi: Luis Suarez ameruhusiwa kufanya mazoezi na Barcelona baada ya CAS kusema FIFA haina uwezo wa kumzuia.
Kombe: Mechi ya kesho ya Barcelona ni ya kombe la Joan Gamper, mechi ya mwisho ya maandalizi ya mwaka.
Mashabiki wa Barcelona wanasubiri kuona Messi na Suarez watakavyocheza pamoja uwanjani

0 comments:
Post a Comment