Saturday, August 16, 2014

Na Baraka Mpenja


Imechapishwa Agosti 16, 2014, saa 12:00 jioni

AZAM FC imefuzu robo fainali ya michuano ya kombe la klabu bingwa ukanda wa Afrika mashariki na kati, maarufu kama Kombe la Kagame baada ya kuifunga Adamma City ya Ethiopia mabao 4-1 katika mchezo uliomalizika jioni hii uwanja wa Nyamirambo mjini Kigali, nchini England.

Mabao ya Azam yamefungwa na John Raphael Bocco ‘Adebayor’, Didier Kavumbagu ‘Kavu’. Kipre Herman Tchetche na Khamis Mcha ‘Vialli’.

Kwa ushindi huo Azam fc wamefikisha pointi nane katika nafasi ya kwanza ya kundi A, lakini wanaweza kushika nafasi ya pili kama Rayon Sport wenye pointi saba watashinda jioni hii.

Wanalamba wametinga robo fainali kwa kushinda mechi mbili na kutoa sare mbili.

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika kwa sare ya bao 1-1 ambapo Azam walikuwa wa kwanza kufunga kupitia kwa Bocco akiunganisha krosi ya Khamis Mcha ‘Vialli’, lakini  Desaleny Bebesh aliisawazishia Adamma katika dakika ya 39.

Katika dakika 55, Kavumbagu alifunga bao la pili akimalizia krosi ya Erasto Nyoni.

Dakika ya 60 Mcha alifunga bao la tatu baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na mlinda mlango wa Adamma na katika dakika ya 74 Tchetche alihitimisha karamu ya mabao.

Mchezo unaondelea muda huu ni baina ya wenyeji Rayon Sport dhidi ya Atlabara kutoka Sudan Kusini.


Kikosi cha Azam FC leo kilikuwa:  Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Gardiel Michael/Said Mourad dk51, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’/Farid Mussa dk61, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Mudathir Yahya dk72, John Bocco ‘Adebayor’, Didier Kavumbangu na Kipre Tchetche.
Waliowakilisha Adama City: Yakoub Fiseha/Yeraswork Terefe dk38, Suleiman Mohamed, Henok Gemtesa, Demetros Wisilase, Mintesinot Kebede, Wonooson Milkesa, Abreham Yisak, Ameha Belete, Abdulkerim Abafogi, Desaleny Debesh/Abiy Beyene dk68 na Benyam Ayele.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video